Nouméa
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Noumea (pia: Numea) ni mji mkuu wa Kaledonia Mpya (Kifaransa: Nouvelle-Calédonie - nuvel kaledoni) ambayo ni eneo la ng'ambo la Ufaransa katika bahari ya Pasifiki.
Mji ulianzishwa mwaka 1854 kwa jina la "Port-de-France" (Bandari ya Ufaransa) kwenye rasi ya kusini ya kisiwa cha Grande Terre. Idadi ya wakazi wake imefikia watu 91.000.
Uchumi wa Noumea hutegema utalii pamoja na migodi ya nikeli.
[hariri] Viungo vya Nje
- Tovuti ya manisipaa ya Noumea (Kifaransa)
Anwani ya kijiografia : 22°16'33"S, 66°27'29"E