N'Djamena

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Ndjamena)


Jiji la N'Djamena
Nchi Chad
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 1,093,492

Ndjamena ni mji mkuu pia mji mkubwa kabisa nchini Chad ikiwa na wakazi 1,093,492 mnamo mwaka 2013.[1]

Ndani ya manisipaa kuna hara au mitaa kumi.

Mtaa wa N'Djamena

Jina[hariri | hariri chanzo]

Zamani mji ulijulikana kwa jina la "Fort Lamy". Tangu mwaka 1973 jina limekuwa Ndjamena, N'Djaména, N'Djamena au Ndjaména.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Mji wa Ndjamena uko mahali ambako mito ya Chari na Logone inaungana. Ng'ambo ya mto uko mji wa Kousseri nchini Kamerun.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Ndjamena ilianzishwa na Mfaransa Émile Gentil tarehe 29 Mei 1900 kama kambi ya kijeshi ikiitwa Fort-Lamy kama kumbukumbu ya kamanda Amédée-François Lamy aliyeuawa vitani kwenye mapigano ya Kousseri siku chache kabla ya kuanzishwa kwa Fort Lamy[2][3] .

Jina lilibadilishwa na rais François Tombalbaye kuwa Ndjamena mwaka 1973. Wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe ya Chad 1979 / 1980 mji uliharibika na wakazi wengi waliondoka mjini lakini katika miaka ya baadaye wengine wengi waliingia.[4]

Wakazi[hariri | hariri chanzo]

Mji ulikua sana na haraka. Huduma za maji, umeme na makao havitoshi tena.

Mwaka * Idadi ya Wakazi

Makabila na vikundi mjini mwaka 1993:

  • Waarabu wa Chad : 11,08 %
  • Ngambay : 16,41 %
  • Hadjeray : 9,15 %
  • Daza : 6,97 %
  • Bilala : 5,83 %
  • Kanembou : 5,80 %
  • Maba : 4,84 %
  • Kanouri : 4,39 %
  • Gor : 3,32 %
  • Kouka : 3,20 %
  • Sar : 2,24 %
  • Barma : 2,10 %

Uchumi[hariri | hariri chanzo]

Ndjamena ni kitovu cha uchumi wa Chad.

Elimu[hariri | hariri chanzo]

Ndjamena ina vyuo na shule mbalimbali kama vile.

Shule za Sekondari (Lycée) :

  • Lycée Félix Éboué (ya serikali)
  • Lycée technique commercial (ya seriali)
  • Lycée du Sacré-Cœur (binafsi - kikatoliki)
  • Lycée-Collège évangélique (binafsi kiprotestant)
  • Lycée Ibnou - Cinna (Kifaransa - Kiarabu)
  • Lycée Roi Faycal (Kiarabu)
  • Lycée Koweitien (Kiarabu)
  • Lycée d'Amérigue (ya serikali)
  • Lycée de Farcha (ya serikali)
  • Lycée Technique Industrielle
  • Lycée du Pont de Chagoua
  • Lycée de Waliya
  • Lycée de La Liberté
  • Lycée de la Gendarmerie, etc.

Vyuo Vikuu (Université) :

créée en 1970
  • Université Roi Fayçal (binafsi - kiislamu)

Taasisi za elimu ya juu (École Supérieure) :

  • ISSED - Institut Supérieur des Sciences de l'Éducation
  • ENAM - École Nationale d'Administration et de Magistrature
  • EIE - École Supérieure d'Électronique et d'Informatique
  • ENASS - École Nationale des Sciences Infirmières et Sociales
  • INJS - Institut Supérieur de la Jeunesse et des Sports
  • ENS - École Normale Supérieure
  • ENTP - École Nationale des Travaux Publics
  • ISTAP - Institut Supérieur des Techniques Appliquées

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Cahiers de l'Afrique de l'Ouest Dynamiques de l'Urbanisation Africaine 2020: Africapolis, Une Nouvelle Géographie Urbaine. OECD. 20 fevereiro 2020
  2. Roman Adrian Cybriwsky, Capital Cities around the World: An Encyclopedia of Geography, History, and Culture, ABC-CLIO, USA, 2013, p. 208
  3. Zurocha-Walske, Christine (2009). Chad in Pictures. Twenty-First Century Books. p. 17. ISBN 978-1-57505-956-3. Archived from the original on 2016-04-30. Retrieved 2015-11-15.  Unknown parameter |url-status= ignored (help)
  4. Samuel Decalo, Historical Dictionary of Chad, Scarecrow, 1987, pp. 229–230

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]