Namba za Kiroma

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Namba za Kiroma (kwa Kiingereza: Roman numerals) ni mfumo wa tarakimu kwa kuandika namba jinsi ulivyokuwa kawaida wakati wa Roma ya Kale na katika mwandiko wa Kilatini. Mfumo huu unaendelea kutumika hadi leo kwa namba za pekee, hasa katika muundo wa orodha ambako mgawanyo ni wa ngazi mbalimbali. Ni kawaida kwa kutofautisha watu wenye jina lilelile, kwa mfano wafalme au mapapa: Malkia Elizabeth II (= wa pili) au Papa Benedikto XVI (= wa kumi na sita).

Herufi za alfabeti kama tarakimu

Jinsi ilivyo katika lugha mbalimbali, hata Waroma walitumia herufi za alfabeti ya Kilatini (ingawa chache) kama tarakimu za kutaja namba pia.

Alama za kimsingi

Herufi chache zilizotumika kwa namba muhimu zaidi, ambazo ziunganishwe kupata namba zote, ni:

I - 1

V - 5

X - 10

L - 50

C - 100

D - 500

M - 1000

Alama Namba Alama Namba Alama Namba Alama Namba Alama Namba Alama Namba Alama Namba
I 1 V 5 X 10 L 50 C 100 D 500 M 1000


Kuunganisha alama za namba

Kujumlisha alama

Namba kubwa zaidi huonyeshwa kwa kuandika alama inayotakiwa upande wa kulia lakini kwa kawaida si zaidi ya mara tatu:
I = 1; II = 2; III = 3, V ni 5 lakini VI ni 6; XX ni 20 lakini XXI ni 21.

Walikuwa na utaratibu wa kutoandika zaidi ya alama tatu ya aina ileile mfululizo. Lakini waliweza kupuuza utaratibu huu pia na kuandika VIIII (9) badala ya IX au XXXX (40) bafala ya XL.

Kupunguza alama

Namba ndogo zaidi huonyeshwa kwa kuandika alama ndogo upande wa kushoto:
V ni 5 lakini IV ni 4 badala ya IIII (inayotokea mara chache); X ni 10 lakini IX ni tisa

Hapa walifuata utaratibu ufuatao: kuweka I moja au X moja au C moja tu kabla ya alama kuwba zaidi; halafu namba hii yatolewa kwenye namba kubwa:

Mfano: IX=9; IXX = 19; IL = 49; LIV=54; XC=90; CD=400; CM=900

I pekee huwekwa kabla ya V au X; X pekee kabla ya L au C; C pekee kabla ya D au M.

Mfano: XCIX (99) lakini siyo IC; CMXCIX (999) lakini siyo IM

Namba mfululizo 1-100

I II III IV V VI VII VIII IX X
1 2 3 4 5 6 7 8 9 10
XI XII XIII XIV XV XVI XVII XVIII XIX XX
11 12 13 14 15 16 17 18 19 20
XXI XXII XXIII XXIV XXV XXVI XXVII XXVIII XXIX XXX
21 22 23 24 25 26 27 28 29 30
XXXI XXXII XXXIII XXXIV XXXV XXXVI XXXVII XXXVIII XXXIX XL
31 32 33 34 35 36 37 38 39 40
XLI XLII XLIII XLIV XLV XLVI XLVII XLVIII XLIX L
41 42 43 44 45 46 47 48 49 50
LI LII LIII LIV LV LVI LVII LVIII LIX LX
51 52 53 54 55 56 57 58 59 60
LXI LXII LXIII LXIV LXV LXVI LXVII LXVIII LXIX LXX
61 62 63 64 65 66 67 68 69 70
LXXI LXXII LXXIII LXXIV LXXV LXXVI LXXVII LXXVIII LXXIX LXXX
71 72 73 74 75 76 77 78 79 80
LXXXI LXXXII LXXXIII LXXXIV LXXXV LXXXVI LXXXVII LXXXVIII LXXXIX XC
81 82 83 84 85 86 87 88 89 90
XCI XCII XCIII XCIV XCV XCVI XCVII XCVIII XCIX C
91 92 93 94 95 96 97 98 99 100