Nabii Isaya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta

Nabii Isaya (kwa Kiyahudi יְשַׁעְיָהוּ, yaani "YHWH anaokoa") alizaliwa katika ufalme wa Yuda (Israeli Kusini mwaka 765 hivi K.K. akatabiri kwa muda usiopungua miaka 40 (740-700 hivi K.K.) akiingilia kati matukio yote ya siasa, ambayo yalikuwa ya kutisha kutokana na nguvu za Waashuru ambao waliangamiza Israeli na kukaribia kufuta hata ufalme wa Kusini.

Maandishi yake yanapendeza kuliko yote ya manabii, hasa upande wa ushairi.

Lakini ukuu wa Isaya uko hasa upande wa imani.

Kuanzia wito wake (6) alitawaliwa na wazo la utukufu wa Mungu na unyonge wa binadamu anayehitaji kutakaswa naye.

Aliwadai wafalme wote wa Yuda wamtegemee Mungu tu, si mataifa yenye nguvu (7:1-8:18; 20:1-6; 22:1-14).

Lakini toka mwanzo aliambiwa hatasikilizwa, hivyo ikambidi atabiri adhabu.

Pamoja na kufanya hivyo alitabiri kuwa Mungu hataangamiza kabisa taifa lake, bali ataacha mabaki yake ambayo yataleta wokovu: katika mabaki hayo Bikira (kwa Ukristo ndiye Bikira Maria) atamzaa Masiya (Yesu Kristo) ambaye ni Emmanueli, yaani Mungu pamoja nasi, mwana wa Daudi ambaye ataleta amani na haki duniani.

[hariri] Viungo vya nje

Vifaa binafsi
Maeneo ya wiki

Vibadala
Vitendo
Urambazaji
Vifaa
Lugha zingine