Mwaprikoti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mwaprikoti
(Prunus armeniaca)
Mwaprikoti unaochanua
Mwaprikoti unaochanua
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Eudicots (Mimea ambayo mche wao una majani mawili)
(bila tabaka): Rosids (Mimea kama mwaridi)
Oda: Rosales (Mimea kama mwaridi)
Familia: Rosaceae (Mimea iliyo na mnasaba na mwaridi)
Jenasi: Prunus
Spishi: P. armeniaca L., 1754

Mwaprikoti ni mti mdogo wa familia Rosaceae. Matunda yake huitwa maaprikoti. Asili ya mti huu haijulikani, kwa sababu ulipandwa sana kabla ya historia. Sikuhizi hupandwa mahali pengi katika kanda za nusutropiki.

Kwa kawaida, jina la mwaprikoti hutumika kwa spishi P. armeniaca, lakini P. brigantina (mwaprikoti-milima), P. mandshurica (mwaprikoti wa Uchina), P. mume (mwaprikoti wa Japani) na P. sibirica (mwaprikoti wa Siberia) yanahusiana sana na matunda yao pia huitwa aprikoti. Matunda haya hayapatikani katika Afrika.

Picha[hariri | hariri chanzo]