Mwanakondoo wa Mungu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Agnus Dei ya Karne za kati katika Basilika la Parenzo, Korasia.
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Mwanakondoo akishika bendera ya Kikristo ni ishara ya Yesu mshindi.

Mwanakondoo wa Mungu ni neno la Injili ya Yohane (1:29, 36) lililotamkwa na Yohane Mbatizaji kumhusu Yesu Kristo ili kumtambulisha kama kafara itakayotolewa kwa ukombozi wa binadamu wote: kwamba atabeba dhambi ya ulimwengu mzima na kuifidia kwa kujitoa kabisa.

Kwa Kilatini neno hilo ni Agnus Dei na linatumika kutajia mchoro wa mwanakondoo mwenye msalaba (au bendera ya msalaba) ukiwa ishara ya Kristo.

Agnus Dei ni pia jina la litania fupi ambayo inaanzia na maneno hayo na kutumika wakati wa Misa padri anapomega hostie takatifu na kuchanganya kipande na umbo la divai lililomo katika kikombe.

Litania fupi ya namna hiyo inapatikana pia katikati ya utenzi maarufu kwa jina la Kilatini "Gloria".

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mwanakondoo wa Mungu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.