Mwada

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mwada ni kata ya Wilaya ya Babati Vijijini katika Mkoa wa Manyara, Tanzania yenye postikodi namba 27202.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi wa kata walihesabiwa kuwa 11,605 [1]. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 16,139 waishio humo.[2]

Wakazi wa Mwada kiuchumi wanajihughulisha na masuala ya kilimo cha mazao mbalimbali kama pamba, ufuta, mahindi, ngwara, maharagwe, alizeti na mbaazi, pamoja na uvuvi mdogo katika ziwa Burunge.

Utalii pia ni sehemu mojawapo ya shughuli za kiuchumi katika eneo hilo kutokana na uwepo wa hifadhi ya Burunge ambayo imepakana na hifadhi ya Taifa ya Tarangire.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Kata za Wilaya ya Babati Vijijini - Mkoa wa Manyara - Tanzania

Arri | Ayalagaya | Ayasanda | Bashnet | Boay | Dabil | Dareda | Duru | Endakiso | Gallapo | Gidas | Kiru | Kisangaji | Madunga | Magara | Magugu | Mamire | Mwada | Nar | Nkaiti | Qameyu | Qash | Riroda | Secheda | Ufana


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Manyara bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mwada kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.