Mungiki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
                                                      

Makala hii ina dalili ya kutungwa kwa kutegemea programu ya kompyuta kama vile "Google translation" au "wikimedia special:content translation" bila masahihisho ya kutosha. Watumiaji wanaombwa kuchunguza tena lugha, viungo na muundo wake. Wakiridhika na hali yake wanaweza kuondoa kigezo hiki kinachoonekana kwenye dirisha la kuhariri juu ya matini ya makala kwa kutumia alama za {{tafsiri kompyuta}} .

Mungiki ni kundi la kisiasa-dini na ni shirika la kihalifu lililopigwa marufuku nchini Kenya.

Jina hilo lina maana ya "umoja wa watu" au "umati" katika lugha ya Kikuyu. Dini hii, ambayo aghalabu ilianza katika miaka ya 1980, ni ya kisiri na hukuza ulinganishi na dini mafumbo. Haswa asili yao na mafundisho yao haielewiki. kilicho wazi ni kwamba hupendekeza kurudi kwa desturi za Kiafrika kama vile kulazimisha tohara ya wanawake.wao hupinga mila za kizungu na mambo yote ambayo wao wanaamini kuwa mitengo ya ukoloni ikiwemo ukisto. itikadi ya kundi hili inahusisha mapinduzi ya kughulumisha,mila za kikuyu,uvunjifu wa sisasa wa kenya, ambao kuonekana kama wazinzi rushwa. Mungiki mara nyingi hujulikana kama Kenya's Cosa Nostra, Yakuza, au Mafia Kenya kutokana na ushirika wake.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Kulingana na mmoja wa waanzilishi wa mungiki, kikundi kilianzishwa mwishoni mwa miaka ya 1980 kama wanamgambo katika maeneo ya miinuko ili kulinda wakulima wakikuyu katika migogoro ya kiardhi na vikosi vya wamasai waliokua waaminifu kwa serikali, ambayo ilikuwa inaongozwa na kabila la waKalenjin wakati huo. Mungiki wanadai kuwa mizizi yake ni katika kutoridhika kunakotokana na ukosefu wa ajira na ukosefu wa ardhi inayotokana na ukuaji wa kasi wa idadi ya watu, kutokana na vijana wengi kukosa ajira hivyokunawavutia na kuwapa hisia na kusudi na utambulisho wa kiutamaduni na kisiasa, kama vile mapato yao.

Waanzilishi aghalabu walianzisha Mungiki kutoka kwa wapiganiaji wa Maumau ambao walipigana na utawala wa kikoloni wa Uingereza. Katika miaka ya 1990, kundi hili lilikua limehamia sehemu ya Nairobi na kukubalika na serikali chini ya Daniel arap Moi na kuanza kudhibiti sekta ya matatu (teksi za kibinafsi). Kuhamia Nairobi kulikuja na maendeleo ya muundo kiini ndani ya kikundi. Kila seli ina wanachama 50 na kila kiini iligawanywa katika platoons tano. kwa kutumia matatu kama kisingizio kundi hili lilihamia maeneo mengine ya biashara,kama vile ukusanyaji takataka, ujenzi, na hata ulinzi. kisha, vitendo vya kundi hili vilisababisha wanasiasa kujihusisha na pupa ili kupata wafuasi wengi.

Uwanaji na ghasia za kikabila[hariri | hariri chanzo]

Mungiki wanapatikana sana katika mtaa wa Mathare, mtaa wa vibanda wa pili mkubwa Nairobi, ambapo umaskini na uhalifu umeenea sana. Kila mkazi wa mitaa ya mabanda hulipa sehemu ya fedha kwa shirika hilo,ili kupata ulinzi dhidi ya wizi na uharibifu wa mali. Aidha, kundi hilo husimamia vyoo vya umma na kulipiza ada kwa ajili ya kutumia vifaa hivyo.

Zaidi ya watu 50 walikufa mwaka wa 2002 katika mapigano iliyowahusisha wamiliki wa matatus na wafuasi wa mungiki katika sehemu la Nairobi peke. katika Mwaka wa 2002 kundi hilo lilipigwa marufuku Februari 2003,kundi hilo liligonga habari kufuatia mapigano ya siku mbili na polisi mjini nairobi ambapo maafisa wawili waliuawa na wafuasi 74 wa kundi la mungiki walitiwa mbaroni. Mwezi Juni mwaka wa 2007, Mungiki walianzisha mauaji katika kampeni ya kutia hofu kwa kuwakata vichwa madereva wa matatu,utingo wa matatu, na wasaliti wa mungiki,kusababisha vikosi vya usalama kuingilia kati ambapo walijitosa kwenye eneo la Mathare. takribani watu 100 waliuawa katika opareshini hiyo.

Itikio la polisi[hariri | hariri chanzo]

Mnamo Novemba 2007, kundi la haki za binadama kiitwacho Oscar Foundation Free Legal Aid Clinic-Kenya kiliripoti kwamba katika miaka mitano hadi Agosti 2007, polisi wa kenya walikuwa wamewaua watu 8,000 katika opareshini dhidi ya kundi la Mungiki, na zaidi ya watu 4,000 bado hawajulikani walipo. Madai haya yalikuwa msingi wa mahojiano, ripoti za polisi, na ilisambazwa sana kote nchini kenya na kwa njia ya kukata rufaa kutoka kwa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu Wakati huo huo,Tume ya Taifa ya haki za Binadamu kenya iliwahusisa polisi kwa utekelezaji wa mauaji ya wanachama 500 wa Mungiki kwa kipindi cha miezi mitano. Polisi walielezea taarifa hizi kama uwongo. Tarehe 5 Machi 2009, Mkurugenzi wa vuguvugu la oscar,Oscar Kamau Kingara na Mratibu wa Programu john paul oulo walipigwa risasi na kuuawa wakielekia kwa mkutano katika afisi za Tume ya Taifa ya Kenya ya Haki za Binadamu mjini Nairobi[11] [12] [13]. Mapema siku hiyo, msemaji wa serikali, Alfred Mutua, alidai hadharani na kukemea vuguvugu hilo kwa kukusanyanyia fegda kundi la mungiki.

mwenyekiti wa Mungiki Maina Njenga aliachiliwa huru tarehe 27 Oktoba 2009 kwa kuwa mauaji juu yake yalikosa ushahidi wa kutosha. baada ya wiki hivi msemaji wa mungiki David Gitau Njuguna alipigwa risari na kuuawa mjini nairobi na mtu asiyetambulikana.

Vita vya mngawanyiko[hariri | hariri chanzo]

katika mwaka wa 2007 mungiki ilidaiwa kungawanyika katika makundi mawili. mauaji ya kuajabisha ya viongozi wakuu wa mungiki yalitokea,licha ya ishara za amani kutoka kwa Waziri Mkuu Raila Odinga, huku polisi wakikanusha kuhusika na mauaji hayo. Mwenyekiti na Mweka Hazina wa Kenya National Youth Alliance (Maina Njenga ubinafsi) alipigwa risasi na kuuawa katika sehemu ya Uplands baada ya ukibishanaji wa magari katika njia kuu ya Nairobi - Naivasha. Kenya National Youth Alliance (KNYA) ni mrengo wa kisiasa wa mungiki. Charles Ndung'u Wagacha na Naftali Irungu walisemekana kuwa njiani kuelekea gereza la Naivasha Prison, ambapo kiongozi wa Mungiki Maina Njenga alikuwa akitumikia kifingo cha jela. familia za wanachama hao wa KNYA waliwalaumu maafisaa wa polisi kwa mauaji hayo. Hata hivyo, msemaji wa polisi Eric Kiraithe alikanusha madai hayo. Polisi wanasema kuwa mauaji ya hivi karibuni ya viongozi wa mungiki ni kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe katika makundi mbalimbali juu ya udhibiti wa fedha na tofauti za kisiasa. Uongozi wa Mungiki, hata hivyo, unakanusha taarifa ya mgawanyiko ndani ya safu zao. Kulingana na familia ya Wagacha na irungu wawili hao walikua wakielekea Naivasha Prison kushauriana na Maina Njenga juu ya uwezekano wa mazungumzo na serikali, yaliopendekezwa na Waziri Mkuu Odinga. Jamaa inasema kwamba vipengele katika serikali ni kutumia polisi kuhakikisha mazungumzo hayafanyiki, hivyo mauaji. Angalau miili ya watuhumiwa 500 wanachama wa Mungiki imegunduliwa tangu katika vichaka nje mwa Nairobi katika kipindi cha mwaka uliopita.

Idara ya Ulinzi[hariri | hariri chanzo]

Mapema mwaka 2003, mara baada ya Mwai Kibaki kuchukua uongozi, serikali iliipa shaba ya juu ya kijeshi siku tatu kuelezea kwa nini landrovers 10 za kijeshi zilipewa kudi lililopingwa marufuku la mungiki. katika kufuatilia uchaguzi mkuu aliyekua kamanda wa kijeshi joseph kibwana aliulizwa kuchunguza kashfa yeye binafsi na kupeana matokeo yake katika ofisi ya rais. Ripoti ingehusisha kwa undani thamani ya magari, nani aliyepeana na kwa sababu gani. kwa wakati huo vyanzo vya kijeshi vilisema kuwa amri ilikua imetolewa na waziri wa Usalama wa Taifa Chris Murungaru alipokutana na jenerali kibwana katika makao makuu ya Idara ya Ulinzi mjini Nairobi. Suala la magari ya landRovers lilianza wakati waziri alifanya ziara yake ya kwanza ya kujijuza kuhusu DoD, mwezi mmoja baada ya NARC kuingia madarakani.

Dr Murungaru, ambaye alikuwa waziri wa usalama aliyeajibikika kwa ajili ya kijeshi, alishtuswa na ripoti kuwa baadhi ya maafisaa wa juu huenda walihusika katika kuwapatia mungiki magari ya landrovers, kama ilivyokiniwa katika ripoti juu ya kashfa hizo zilizoripotiwa na gazeti la daily nation. wanachama wa juu wa DoD waliohusika inasemekana walifanya mazungumzo ya siri muda mfupi kabla ya Dr Murungaru kuwasili kupanga la kufanya baadaye. Ripoti na matokeo yake haijawahi kuelizewa umma.

Idara ya Ulinzi ilibandilishwa na kuwa Wizara ya Ulinzi na inaongozwa na hon Yusuf Haji.

Ripoti ya Waki[hariri | hariri chanzo]

Kulingana na tume iliyoanziswa 2008 kuchunguza ghasia za baada ya uchanguzi iliripotiwa kuwa wanachama wa mungiki walihusika na uchochezi wa ghasia. Ripoti ya Waki inasema kwamba mkutano ulifanyika kwenye ikulu kuratibu kisasi dhidi ya Wajaluo na Wakalenjin.

Ripoti pia inapendekeza kwamba watu waliochochea, wakiwemo pamoja na mawaziri, wabunge na wafanyabiashara maarufu kushitakiwa katika mahakama ya nchini au Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).

Uhamishoni[hariri | hariri chanzo]

Inasemekana kwamba wanachama wa zamani wa mungiki wametoroka nchini na kutafuta maficho kwa sababu dhehedu hilo halikubali usaliti Pia kulikuwa na matukio mengi ya kulazimishwa kujiunga na kundi hilo ambayo ilipanda vikubwa baada ya uchaguzi wa rais wa 2007.

Sintofahamu[hariri | hariri chanzo]

  • Kumekuwa na madai yasiyodhibitiswa kwamba Mungiki ina viungo katika serikali ya KANU ya zamani na baadhi ya wabunge katika serikali ya sasa. ama kwa hakika , kwa sababu ya ibada ya usiri uliokithiri, ni machache yanajulikana kuhusu uanachama wake au uongozi wake.
  • Wanaokubali bini hii humaliza kwa kuapa kiapo "nitakufa nikilisaliti au kufichua siri"
  • Wanachama wengi wanahisi ya kuwa katika urefu wa ushawishi wake, kikundi kinaweza kudai kuwa uwanachama wake ni 500000 na hupokea kiasi cha pesa. wakenya wengi wanajadili kama ushawishi wa kundi hili unadidimia au unaongezeka mjini nairobi.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

  • Kenya National Youth Alliance - mrengo wa kisiasa wa Maina Njenga wa Mungiki.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]