Muhutwe

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Muhutwe ni jina la kata ya Wilaya ya Muleba katika Mkoa wa Kagera, Tanzania yenye postikodi namba 35505 [1]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 11,491 waishio humo.[2].

Wakazi wa Muhutwe wanaishi kwa kutegemea shughuli za kilimo na ufugaji. Chakula kikuu ni ndizi. Wanalima kahawa kama zao la biashara. Muhutwe kwa upande wa magharibi inapakana na mto wa kudumu unaoitwa Mto Ngono. Pamoja na kuwa na uwezekano mkubwa wa kukuza uchumi wa wananchi wanaouzunguka bado fursa hii haijatumiwa ipasavyo kwani mpaka sasa mto huu hauna shughuli zozote za maendeleo.

Mto Ngono ni kivutio kikubwa cha utalii kutokana na kuwa na wanyama wakubwa kama kiboko.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2018-08-05. Iliwekwa mnamo 2018-02-01.
  2. Sensa ya 2012, Kagera - Muleba-District-Council
Kata za Wilaya ya Muleba - Mkoa wa Kagera - Tanzania

Biirabo | Bisheke | Buganguzi | Buhangaza | Bulyakashaju | Bumbire | Bureza | Burungura | Goziba | Gwanseli | Ibuga | Ijumbi | Ikondo | Ikuza | Izigo | Kabirizi | Kagoma | Kamachumu | Karambi | Kasharunga | Kashasha | Katoke | Kerebe | Kibanga | Kikuku | Kimwani | Kishanda | Kyebitembe | Mafumbo | Magata Karutanga | Mayondwe | Mazinga | Mubunda | Muhutwe | Muleba | Mushabago | Ngenge | Nshamba | Nyakabango | Nyakatanga | Ruhanga | Rulanda | Rutoro


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kagera bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Muhutwe kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.