Mozaiki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mtindo wa Mozaiki ya Kiislamu katika kanisa kuu la Monreale (Sisilia - karne ya 12)

Mozaiki (mosaiki; ) ni mtindo wa pekee wa uchoraji picha unaotumia vipande vidogo vya kioo cha rangi au vigae vya rangi mbalimbali vinavyounganishwa kuwa picha. Kunawezekana pia kutumia vipande vya vitu vyovyote vyenye rangi vinavyoweza kuunganishwa kuwa picha.

Mozaiki ya mawe mweupe na meusi kwenye sakafu ya nyumba ya Ugiriki ya Kale

Yaliyomo

[hariri] Chanzo cha mtindo wa mozaiki

Mtindo huu ulionekana mara ya kwanza huko Phrygia (katika Uturuki ya leo) iliyokuwa sehemu ya ustaarabu wa Ugiriki ya Kale. Mawe ya rangi nyeupe na nyeusi yalipangwa ukutani au kwneye sakafu kuwa tarakibu.

Kichwa cha mungu Amfitriti kutoka nyumba ya Herkulaneo ya karne ya 1 KK

Baadaye Wagiriki na zaidi Waroma waliendelea kuongeza rangi na kutunga picha kamili si tarakibu tu kwenye kuta za nyumba. Maghofu ya Kiroma yanaonyesha mifano mingi iliyodumu hadi leo.

[hariri] Mozaiki za Bizanti na za Waarabu

Sanaa ya mozaiki iliendelezwa katika ustaarabu wa Bizanti. Wabizanti walipamba makanisa, majumba ya kifalme na pia nyumba za matajiri kwa mozaiki nzuri kabisa.

Waarabu Waislamu walipotwaa shemu kubwa za milki ya Bizanti waliendelea kuwaajiri wasanii Wabizanti wakipamba misikiti kama msikiti wa Umawiya huko Dameski au majumba ya masultani.

Baadaye walikuwa mafundi Waislamu waliopamba makanisa na nyumba katika Italia ya kusini.

[hariri] Mozaiki leo

Mtindo wa mozaiki umeaendelea kutumiwa hadi leo. Kwa kawaida mozaiki inaendelea kuwa picha inayounganishwa kwa njia ya kudumu na ukuta au safau ya jengo fulani. Inawezekana pia kuifunga katika fremu na kubadilisha mahali pake lakini picha za mozaiki huwa nzito.


[hariri] Mifano ya mozaiki

[hariri] Viungo vya Nje

WikiMedia Commons
WikiLettreMini.svg Makala hiyo kuhusu "Mozaiki" inatumia neno ambalo si kawaida na matumizi yake ni jaribio kwa jambo linalotajwa.
Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao.

Kamusi za Kiswahili ama zinatofautiana kuhusu matumizi ya neno hili au hazieleweki au hazina neno kwa jambo linalojadiliwa.