Moyo kushindwa kusambaza damu kwa ghafla

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Uvimbe wa mapafu wa ghafla. Kumbuka moyo ulozidishwa ukubwa, mgawanyo wa juu wa vascula(mduara), na mdogo wa pande zote za mtiririko wa damu kwenye membrini zilizoko kwenye mapafu (mshare).

{moyo kushindwa kusambaza damu kwa ghafla{/0} (ADHF) ni sababu ya kawaida na kubwa ya kusababisha kushindwa kupumua kwa ghafla.

visababishi[hariri | hariri chanzo]

usugu wa kushindwa kwa uthabiti wa moyo unaweza kiulahisi kusababisha kushindwa kwa usambazaji wa damu. Hii kwa kawaida sana ni matokeo ya ugonjwa ulotokea karibuni (kama vile {)kichomi,{/0} uinifarakti wa maiokaridiali (mshtuko wa moyo), pumu, shinikizo la damu lisilozibitiwa, au mgonjwa kushindwa kudumisha udhibiti wa maji, chakula au dawa. [1] Sababu nyingine ambazo ni vizuri kutambuliwa na zinazochochea ni pamoja na upungufu wa damu na utoaji wa kiwango cha juu cha homoni za koromeo ambazo zinaleta maumivu ya ziada kwenye misuli ya moyo. Utumiaji mwingi wa vimiminika au ulaji wa chumvi, na dawa ambayo husababisha uwekaji wa maji kama vile NSAIDs na thiazolidinedione, pia inaweza kuchochea moyo kushindwa kusambaza damu . [2]

uinifarakti wa maiokardia uliomkali unaweza kuchochea moyo kushindwa kusambaza damu kwa ghafla na itapelekea kuibuka kwa kurejea kwa mtiririko wa damu katika viungo na damu kushindwa kufunga, kupitisha damu bila kupitia korinari, au kipandikizi cha upenyo wa ariteri ya coronari.

Tiba[hariri | hariri chanzo]

katika moyo kushindwa kusambaza damu kwa ghafla, lengo la mara moja ni kuanzisha tena uingizaji damu wa kutosha na upelekaji wa oksijeni kwa viungo vyote vya mwisho. Hii inahusu kuhakikisha kwamba njia ya hewa, upumuaji, na mzunguko wa damu ni wa kutosha.

Oksijeni[hariri | hariri chanzo]

oksijeni ya ziada inaweza kutumiwa iwapo kama hypoxemia yaani uwepo wa oksijeni kidogo kwenye moyo upo asasi inayoshuhurikia,Kushindwa kwa moyo ya Marekani, hata hivyo, imependekeza kuwa njia hiyo isitumiwe mara kwa mara. [3]

matibabu ya dawa[hariri | hariri chanzo]

Tiba ya awali ya moyo kushindwa kusambaza damu kwa kawaida inajumuisha baadhi ya muunganiko wa vipanuzi vya mishipa ya damu kama vile nitrogiliserine yaani dawa ya maji ya kuzibua mishipa ya damu, au dawa ya kuongeza mkojo kama vile furosemide, na upenyeshaji wa msukumo hasi usioonekana (NIPPV).o;

Hata kama dalili ya kushindwa kwa Moyohaionekani kwa sasa, dawa inaweza kutumika kwa kutibu dalili ambazo zimezoeleka. Dawa hizo zinakazi ya kudhibiti dalili hizi ikiwa ni pamoja na kutibu matatizo mengine ya afya ambayo yanaweza kuwepo sasa. Yanaweza kufanya kazi ya kuboresha ubora wa maisha,kushusha chini kuendelea kwa kushindwa kwa moyo na kupunguza hatari ya matatizo mengine ambayo yanaweza kutokea kutokana na kushindwa kwa moyo. Ni muhimu sana kutumia madawa sahihi hasa kama yalivyoagizwa na daktari.

Idadi kubwa ya dawa mbalimbali zinahitajika kwa ajili ya watu ambao wanapatwa na hali ya kushindwa kwa moyo. aina ya kawaida ya dawa ambazo zinaagizwa kwa wagonjwa wa kushindwa kwa moyo ni pamoja na dawa za kuzuia ACE, dawa za kupanua mishipa ya damu, dawa za kusaidia mwenendo wa moyo,dawa ya kuyeyusha damu, dawa ya kuvunja mpito wa kalisi, na dawa ya kupunguza kolesto. Kulingana na aina ya uharibifu ambao mgonjwa ameteseka nao na kusababisha msingi wa kushindwa kwa moyo, yeyote ya madaraja ya madawa hayo au mchanganyiko wake unaweza kutumika. Wagonjwa wenye matatizo ya moyo kusukuma damu watatumia mjumuisho wa dawa tofauti na zile wanazotumia wale ambao wanakabiliwa na matatizo ya moyo kujaa. Uwezekano wa hatari ya mwingiliano wa dawa unaweza kutokea wakati dawa tofauti zinapochanganywa pamoja na kufanyakazi dhidi ya kila mmoja. [4] dawa zote zina madhara yake. Nyingi juu-ya-zinazotumika kama dawa zinaweza kusababisha hali ya kushindwa kwa moyo kuwa mbaya zaidi.

Vitanuzi[hariri | hariri chanzo]

Nitreti kama vile nitrogiliserini mara nyingi hutumika kama sehemu ya matibabu ya awali kwa ajili ya ADHF.

chaguo jingine ni nesiritidi, ingawa ni lazima tu kuchukuliwa kama matibabu ya kawaida yamekuwa hayana mafanikio au imeonekana kama ni ghali zaidi kuliko nitrogiliserini na haijawahi kuonesha kuwa na faida yoyote ya ziada.

Dawa ya kuongeza mkojo[hariri | hariri chanzo]

Kushindwa kwa moyo kwa kawaida kunahusishwa na hali ya ujazo mkubwa wa kupitiliza. Basi wale walio na ushahidi wa maji kuwa mengi wanatakiwa wapatiwe matibabu ya awali ya kitanzi cha kuzuia kuongezeka mkojo. Kutokana na kukosekana kwa dalili za kiwango cha chini cha msukumo wa damu ndani ya mishipa baruti kari mara nyingi hutumika pamoja na tiba ya kuongeza mkojo kuboresha dalili msongamano. [3]

Hali ya ujazo inatakiwa iendelee kufanyiwa tathmini ya kutosha. Baadhi ya wagonjwa wa ugonjwa wa kushindwa kwa moyo wenye usugu wa dawa ya kuongeza mkojo wanaweza kuwa na ongezeko la mkojo zaidi. Katika matukio ya mtanuko wa moyo pale moyo unapopokea damu kushindwa kufanya kazi yake vizuri pasipo kusinyaa kwa moyo pale unapopeleka damu kwenye mishipa kushindwa kufanya kazi yake vizuri,kimiminika kikirejeshwa katika hali njema inaweza kwa kweli kuboresha mzunguko na kupunguza kiwango cha moyo, ambacho kitawezesha vyumba vya chini vya moyo kuwa na muda zaidi wa kujaza. Hata kama mgonjwa anajawa na maji mengi katikati ya seli za tishu, kimiminika kikilejeshwa katika hali njema inaweza kuwa njia ya kwanza ya matibabu kama mgonjwa ana msukumo mdogo wa damu. mgonjwa huweza kwa ukweli kutumia usambazaji uliopo wa ujazo kutokea ndani ya mishipa ya damu, ingawa endapo msukumo mdogo wa damu ni kutokana na mshtuko au ugonjwa wa moyo, maji ya ziada yanaweza kufanya hali kuwa mbaya. Endapo mgonjwa anamzunguko wa ujazo wa kutosha, lakini kuna mwendelezo wa ushahidi wa kutotosha uingizaji wakimiminika kwenye mwisho wa mishipa ya fahamu, athari ya msinyao wa misuli unaweza kuonekana. Katika hali fulani, kifaa cha kusaidia chumba cha moyo cha kushoto (LVAD) huwa ni lazima.

Mara baada ya mgonjwa kutulia, tahadhari zinaweza kugeuka nakuwa kutibu uvimbe wa mapafu na kuboresha hewa. dawa ya kuchochea mkojo inayowekwa ndani ya mishipa kwa ujumla ni njia ya awali. Hata hivyo, wagonjwa walio kwenye matumizi ya muda mrefu ya mfumo wa dawa za kuongeza mkojo wanaweza kuwa wavumilivu, na lazima dozi kuendelea kuongezeka. Kama viwango vya juu vya dawa inayotumika kuchochea mkojo ni duni,njia ya kuingiza dawa kwa kutumia sindano ndani ya mishipa au kuendelea kuongeza dawa kupunguza majimaji ndani ya mishipa inaweza kuwa sahihi. kitanzi cha dawa ya kuongeza mkojo hizi huweza kuwa pamoja na dawa za kuongeza mkojo zinazochochea mtiririko mkubwa wa maji kama vile metolazone ya kumeza au klorothiazide ya kuweka kwenye mishipa kwa ajili ya athari ya dawa kwenye mishipa. maandalizi ya kuweka dawa ndani ya mishipa yanapendelewa zaidi kwa sababu ya nanma nyingi za kuchagua zinazotabirika. Wakati mgonjwa amezidiwa sana na maji, yanaweza kuendeleza uvimbe kwenye utumbo pia, ambao unaweza kuathiri ufyonzwaji wa dawa wa ndani.

Matibabu mengine[hariri | hariri chanzo]

ACE inayozuia madhara ya kemikali na ARBs

Ufanisi na usalama wa ACE inayozuia madhara ya kemikali na vivunjivu vya kithibiti vipokezi haraka katika ADHF haijawahi kuwa masomo lakini kinadharia zinadhuru. mtu anapaswa kuwa amedhibitiwa kabla ya tiba aidha ya haya makundi ya dawa kuanza. [5]

vizuizi vya -B

Vizuizi vya-B vikisimamishwa au vikipunguzwa kwa watu wenye shinikizo la chini la damu yaani BP. Hata hivyo muendelezo wa vizuizi vya-B kama shinikizo la damu ni la kutosha vinaweza kuwa sahihi. [6]

Mawakala wa kuathiri misuli

kuathirika kwa misuli inatokea kama msukumo mdogo wa damu (BP <90) upo.

dawa za usingizi

Dawa za usingizi kijadi zinatumiwa katika matibabu ya uvimbe wa mapafu wa ghafla unaotokana na kushindwa kwa moyo kwa ghafla. Mapitio ya 2006 hata hivyo yalipata ushahidi kidogo kusaidia hili zoezi. [7]

Uingizaji hewa[hariri | hariri chanzo]

Mwendelezo chanya wa msukumo wa njia za hewa unaweza kutumika kwa kutumia barakoa ya uso; hii imeonekana kuboresha dalili kwa haraka zaidi kuliko tiba ya oksijeni peke yake, [8] na ina katika baadhi ya masomo imeonyeshwa kupunguza hatari ya kifo. [9] [10] Hali mbaya yakushindwa kupumua inahitaji matibabu na kuweka neli ndani ya koo na uingizaji hewa kwa kutumia mitambo.{

uchujaji wa hali ya juu[hariri | hariri chanzo]

Uchujaji wa hali ya juu unaweza kutumika kuondoa maji maji kwa watu wenye ADHF yanayohusiana na kushindwa kwa figo. Mafunzo yamegundua kuwa huduma za afya zitapungua matumizi kwa siku ya tisini. [11]

Upasuaji[hariri | hariri chanzo]

Baadhi ya matukio itahitaji ushauri unaoibuka na upasuaji wa kifua na moyo. Kushindwa kwa moyo kutokana na urudishaji damu ukiwa wa ghafla unatakiwa upasuaji wa dharura uanaohusiana na vifo kwa wingi. Kushindwa kwa Moyo huweza kutokea baada ya kupasuka kwa aneurisimu ya chumba cha moyo[[]]. Hayo huweza kutengenezwa baada ya uinifarakti wa maiokaridiali,utakuwa umesababisha kizuizi cha damu inayoathiri moyo,kama mpasuko katika ukuta huru. Kama mpasuko uko kwenye septamu ya ndani ya chumba cha moyo, inaweza kuunda ulemavu wa septali ya chumba cha moyo. Sababu nyingine za kuzuia damu inayoathiri moyo pia zinahitaji kuingilia kati kwa kutumia upasuaji, ingawa matibabu ya haraka pembeni mwa kitanda yanaweza kutosha. Ni lazima pia kuamua kama mgonjwa alikuwa na historia ya ugonjwa wa moyo tangu kuzaliwa kwa jinsi mara kwa mara anavyopata matatizo ya kuathiriwa kwa ndani kwa umbo la moyo pamoja na tishu hai za bandia na sehemu zinazopitisha damu nje ya mfumo wake ili kuendeleza uharibifu, na hivyo kusababisha moyo kushindwa kusambaza damu kwa ghafla.

Katika baadhi ya matukio, madaktari hupendekeza upasuaji kutibu tatizo la msingi linalo pelekea kushindwa kwa moyo. [12] Taratibu tofauti zinapatikana kulingana na kiwango cha ulazima na ni pamoja na upasuaji wa ariteri ya kolonali ili kurejesha mfumo wa damu kutengeneza valvu za moyo au uingizwaji, au upandikizwaji wa moyo. Wakati wa taratibu hizi, vifaa kama vile pampu za moyo, kiratibisha mapigo ya moyo, au mashine ya kustua moyo inaweza kupandwa. Matibabu ya maradhi ya moyo yanabadilika kwa kasi na hivyo Matibabu mapya kwa ajili ya matibabu ya kushindwa kwa moyo kwa ghafla matibabu yameanzishwa kuokoa maisha zaidi kutokana na mashambulizi hayo mkubwa. [13]

upasuaji wa kurejesha njia ya damu unafanywa kwa kuondoa mshipa kutoka kwenye mkono, mguu, au kifua na kubadilisha mshipa ulokuwa umefungwa katika moyo. Hii inaruhusu damu kutiririka kwa uhuru zaidi kwa kupitia moyo. Kukarabati valvu ni pale valvu inayosababisha kushindwa kwa moyo inapofanyiwa matengenezo kwa kuondoa tishu zilizozidi ambazo zinasababisha msongamano mkubwa. Katika baadhi ya matukio, anuloplasiti inatakiwa kuchukua nafasi ya pete inayozunguka valvu. Kama ya marekebisho ya valvu hayawezekani,inabadilishwa na kuweka valvu ya bandia. Hatua ya mwisho ni moyo mbadala. Iwapo hali mbaya sana ya kushindwa kwa moyo inakuwepo na madawa au taratibu zingine za kutibu moyo si za ufanisi, moyo wenye ugonjwa unahitaji kubadilishwa.

Utaratibu mwingine wa kawaida unaotumiwa kutibu wagonjwa wa kushindwa kwa moyo ni angioplasiti. Ni utaratibu unaotumika kuboresha dalili za ugonjwa wa ariteri za koronari (CAD), kupunguza uharibifu wa misuli ya moyo baada ya moyo kushambuliwa, na kupunguza hatari ya kifo kwa wagonjwa wengine. [14] utaratibu huu unafanywa kwa kuweka puto katika moyo ili kufungua ariteri ambayo imefungwa na atherosklerosisi yaani ugonjwa wa ariteri au ujenzi wa plaque juu ya kuta za ariteri. Wagonjwa ambao wanauzoefu wa kushindwa kwa moyo kwa sababu ya CAD au mashambulizi ya hivi karibuni ya moyo, wanaweza kufaidika kutoka utaratibu huu.

kiratibisha mapigo ya moyo yaani pacemaker ni kifaa kidogo ambacho huwekwa ndani ya kifua au tumbo kusaidia kudhibiti mapigo ya moyo yasiyo sahihi. [15] Vinafanya kazi kwa kupeleka mapigo ya umeme kwenda kwenye moyo kwa kuharakisha moyo kupiga kwa kiwango kitakachoonekana kuwa cha kawaida na zinatumika kutibu wagonjwa wa mapigo ya moyo kutokuwa mazuri yaani arrhythmias. Zinaweza kutumika kutibu moyo ambao uko kwenye kundi la tachikaridia ambao unapiga kwa haraka, au bradikaridia ambao unapiga polepole mno.

Tazama Pia[hariri | hariri chanzo]

  • Ugonjwa wa mshtuko wa moyo
  • Utaratibu wa Dori
  • Urudiaji wa undaji wa ventriko
  • Kuzidiwa kwa kimiminika

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Fonarow GC, Abraham WT, Albert NM, et al. (Aprili 2008). "Factors Identified as Precipitating Hospital Admissions for Heart Failure and Clinical Outcomes: Findings From OPTIMIZE-HF". Arch. Intern. Med. 168 (8): 847–854. PMID 18443260. doi:10.1001/archinte.168.8.847. 
  2. Nieminen MS, Böhm M, Cowie MR, et al. (Februari 2005). "Executive summary of the guidelines on the diagnosis and treatment of acute heart failure: the Task Force on Acute Heart Failure of the European Society of Cardiology". Eur. Heart J. 26 (4): 384–416. PMID 15681577. doi:10.1093/eurheartj/ehi044. 
  3. 3.0 3.1 Heart Failure Society Of America (Februari 2006). "Evaluation and management of patients with acute decompensated heart failure". J. Card. Fail. 12 (1): e86–e103. PMID 16500576. doi:10.1016/j.cardfail.2005.11.017. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2008-11-04. Iliwekwa mnamo 2010-10-14.  Unknown parameter |= ignored (help); Unknown parameter |https://web.archive.org/web/20081104053735/http://guideline.gov/summary/summary.aspx?doc_id= ignored (help)
  4. [6] ^ Dawa za kawaida Zinazotumika kutibu Kushindwa kwa Moyo Ushirika wa Moyo Marekani. Iliyotolewa tena 2007/01/28.
  5. Gheorghiade M, Zannad F, Sopko G, et al. (Desemba 2005). "Acute heart failure syndromes: current state and framework for future research". Circulation 112 (25): 3958–68. PMID 16365214. doi:10.1161/CIRCULATIONAHA.105.590091. 
  6. Jondeau G, Neuder Y, Eicher JC, et al. (Septemba 2009). "B-CONVINCED: Beta-blocker CONtinuation Vs. INterruption in patients with Congestive heart failure hospitalizED for a decompensation episode". Eur. Heart J. 30 (18): 2186–92. PMID 19717851. doi:10.1093/eurheartj/ehp323. 
  7. "BestBets: Does the application of opiates, during an attack of Acute Cardiogenic Pulmonary Oedma, reduce patients' mortality and morbidity?". Iliwekwa mnamo 6 Desemba 2008. 
  8. Gray A, Goodacre S, Newby DE, Masson M, Sampson F, Nicholl J (Julai 2008). "Noninvasive ventilation in acute cardiogenic pulmonary edema". N. Engl. J. Med. 359 (2): 142–51. PMID 18614781. doi:10.1056/NEJMoa0707992. 
  9. Masip J, Roque M, Sánchez B, Fernández R, Subirana M, Expósito JA (Desemba 2005). "Noninvasive ventilation in acute cardiogenic pulmonary edema: systematic review and meta-analysis". JAMA 294 (24): 3124–30. PMID 16380593. doi:10.1001/jama.294.24.3124. 
  10. Peter JV, Moran JL, Phillips-Hughes J, Graham P, Bersten AD (Aprili 2006). "Effect of non-invasive positive pressure ventilation (NIPPV) on mortality in patients with acute cardiogenic pulmonary oedema: a meta-analysis". Lancet 367 (9517): 1155–63. PMID 16616558. doi:10.1016/S0140-6736(06)68506-1. 
  11. Costanzo MR, Guglin ME, Saltzberg MT, et al. (Februari 2007). "Ultrafiltration versus intravenous diuretics for patients hospitalized for acute decompensated heart failure". J. Am. Coll. Cardiol. 49 (6): 675–83. PMID 17291932. doi:10.1016/j.jacc.2006.07.073. 
  12. [22] ^ [1]Matibabu na dawa kwa ajili ya Kushindwa kwa Moyo/1} Kliniki ya Mayo. Iliyotolewa tena 2007/01/28.
  13. [23] ^ Kushindwa kwa Moyo kwa Ghafla Ufafanuzi Na Uratibu Ilitolewa tena 2010/01/22
  14. [24] ^ Angioplasti ya Coronari Ni Nini Taifa na Taasisi ya Taifa ya Moyo Mapafu na Damu. Iliyotolewa tena 2007/01/28.
  15. [25] ^ [2]Angioplasti ya Coronari Ni Nini/1}Taasisi ya Taifa ya Moyo Mapafu na Damu. Iliyotolewa tena 2007/01/28.