Mlinganyo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mlinganyo ni kama mizani; ni muhimu ya kwamba hatua zinatekelezwa pande zote mbili kwa shabaha ya kurahisisha mlinganyo

Mlinganyo (kutoka kitenzi "kulinga") katika hisabati (aljebra) ni kauli inayosema kuwa viwango viwili ni sawa yaani vinalingana. Milinganyo yote hutumia alama ya "="

kama vile 2 + 3 = 5

ambayo inasema "mbili ongeza tatu inalingana na tano".

Mlinganyo wa undani zaidi unatumia alama kwa viwango visivyojulikana awali na vinapaswa kugunduliwa,

Mfano :

3x + 3 = 9

Suluhisho linapatikana kwa kufuata hatua zinaopeleka "x" peke yake upande mmoja wa mlinganyo. Hatua hizi zinapaswa kuwa sawa pande zote mbili:

  • 3x + 3 - 3 = 9 -3 (ondoa 3 pande zote mbili)
  • 3x = 6
  • 3x : 3 = 6 : 3 (gawanya kwa 3 pande zote mbili)
  • x = 2

Hapo kazi ni kujua maana ya x ni nini ambayo ni 2 katika mfano huu.

Makala hii kuhusu mambo ya hisabati bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mlinganyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.