Mkutano wa mawaziri wa Afrika kuhusu mazingira

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mkutano wa mawaziri wa Afrika kuhusu mazingira (African Ministerial Conference on the Environment kifupi AMCEN) ni ushirikiano wa mawaziri husika wa nchi za Afrika.

Mawaziri hao walikutana mara ya kwanza mwaka 1985 mjini Kairo, Misri. Baadaye mkutano ulianzishwa kama taasisi ya kudumu mwenye shabaha ya

AMCEN ilishiriki katika maandalizi ya mradi wa New Partnership for Africa 's Development (NEPAD) upande wa mazingira.

Mkutano unashirikiana na Mradi wa Umoja wa Mataifa Kuhusu Mazingira (UNEP).

Masahihisho ya Mkataba wa Afrika kuhusu hifadhi ya mazingira na maliasili yaliandaliwa katika AMCEN.

Mkutano wa mawaziri unafanyika kila baada ya miaka miwili. Ofisi ya UNEP-Afrika inatoa huduma ya ofisi ya kudumu kwa AMCEN pia.