Mkutano wa Vienna

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mkutano wa Vienna (Uchoraji na Jean-Baptiste Isabey, 1819.

Mkutano wa Vienna ulikuwa mkutano wa kimataifa wa nchi za Ulaya uliofanyika mjini Vienna (Austria) kati ya 18 Septemba 1814 hadi 9 Juni 1815. Maazimio ya mkutano huu yalichora mipaka ya Ulaya kwa miaka mingi ya mbele.

Shabaha ya mkutano wa Vienna[hariri | hariri chanzo]

Shabaha kuu ya mkutano ilikuwa kujenga utaratibu mpya katika Ulaya baada ya vita za Napoleoni. Katika miaka iliyotangulia mtawala huyu wa Ufaransa aliwahi kuvuruga nchi zote za Ulaya bara; alifuta madola makubwa na madogo na kuunda nchi mpya. Mabadiliko haya yalitazamiwa kuwa si halali na baada ya mwisho wa Napoleoni viongozi wa mataifa waliona haja ya kurudisha utaratibu wa kale pale ulipowezekana au kuunda utaratibu mpya uliolingana na haki.

Pamoja na kuchora upya mipaka ya Ulaya mkutano uliangalia pia mambo yafuatayo:

Mahudhurio na mataifa makuu[hariri | hariri chanzo]

Waliohudhuria walikuwa wawakilishi wa madola, nchi, mataifa, miji ya kujitawala jumla 200 za Ulaya. (Wakati ule nchi kama Ujerumani au Italia zilikuwa na madola mengi ya kujitegemea kabisa ndani zao).

Washindi wa vita dhidi ya Napoleon walikuwa na nafasi kuu na kufanya maazimio muhimu kati yao. Ndio Urusi, Uingereza, Austria na Prussia, pamoja na ufalme uliotengenezwa upya wa Ufaransa. Waliamua maswali muhimu pamoja.

Kwa mambo mengine walishauriana na wawakilishi wa maeneo yaliyohusika, hasa na Hispania, Ureno, Uswidi na madola ya Ujerumani kama vile Hanover, Bavaria na Württemberg.

Wanasiasa muhimu zaidi walikuwa

Mipaka ya Ulaya baada ya Mkutano wa Vienna

Agenda[hariri | hariri chanzo]

Mkutano ulishughulika agenda zake katika kamati mbalimbali kama vile mambo ya Ulaya, mambo ya Ujerumani, swali la ugawaji wa maeneo ya madola yasiyorudishwa, swali la uhuru wa usafiri kwenye mito ya kimataifa na swali la biashara ya utumwa.

Katika matokeo muhumi ni hizi:

  • Ufaransa ulirudishwa katika mipaka ya 1789 ikaacha madai kwa maeneo yote yaliyotekwa chini ya Napoleon.
  • katika Ujerumani madola 300 yaliyokuwepo kabla ya Napoleoni hayakurudishwa; maeneo yaliunganishwa katika madola 40 makubwa zaidi.
  • Madola ya Ujerumani yaliunganishwa katika shirikisho bila serikali kuu. Austria ikapewa nafasi ya mwenyekiti. Madola makubwa ya Austria na Prussia yalikuwa wanachama na sehemu za kale ya maeneo yao; maeneo yao yaliyokuwa nje ya mipaka ya Dola la Ujerumani la Kale yalibaki nje. Watawala wa Hanover, Saksonia na Württemberg walipewa cheo cha mfalme.
  • Poland iligawiwa upya kati ya Urusi, Austria na Prussia.
  • Uholanzi ilirudishwa ikapewa maeneo ya jirani yaliyokuwa zamani chini ya Austria na kuitwa "Ufalme wa Maungano ya Uholanzi".
  • Dola la Papa lilirudishwa katika Italia ya Kati.
  • Austria iliongezewa maeneo katika Italia ya Kaskazini.

Azimio kuhusu Biashara ya watumwa[hariri | hariri chanzo]

Uingereza ilishawishi madola makubwa ya kutamka azimio la kupinga biashara ya watumwa. Azimio hili halikugusa swali la utumwa lenyewe. Azimio la Vienna lilikuwa muhimu kwa mapatano yaliyofuata kati ya Uingereza na nchi mbalimbali ya kuharamisha biashara ya watumwa, kwa mfano na Ufaransa, Hispania na Ureno.

Hali halisi biashara iliendelea kwa muda mrefu kwa sababu serikali za Hispania na Ureno ziliendelea kuvumilia biashara hii hasa kati ya Afrika na kolonia zao zilizoendelea kutumia kazi ya watumwa katika uchumi wa mashamba ya miwa na mazao mengine. Lakini azimio la Vienna ilikuwa hatua muhimu katika harakati ya kukomesha biashara ya watumwa na mshishowe utumwa mwenyewe kwa upande wa mataifa ya Ulaya.