Mkoa wa Njombe
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mkoa mpya wa Njombe umechukua eneo lote la kusini la Mkoa wa Iringa katika Tanzania
Wilaya za Mkoa wa Iringa na mikoa jirani hadi mwaka 2010.
Mkoa wa Njombe ni moja kati ya mikoa mipya Tanzania, ukiwa umeanzishwa rasmi mwaka 2012. Umepakana na mikoa ya jirani ya Morogoro, Ruvuma, Mbeya na Iringa.
Mwaka 2002 katika eneo hilo kulikuwa na wakazi 654,929 [1] katika wilaya zifuatazo: Makete (wakazi 106,061), Njombe (wakazi 420,348), Ludewa (wakazi 128,520).
Kutokana na hadhi mpya, wilaya ya Njombe imegawanyika kati ya ile ya mjini na ile ya vijijini. Pia, mwezi wa Machi 2012, imeanzishwa wilaya ya Wanging'ombe.
Makao makuu yako Njombe mjini.
Wenyeji wa mkoa ni hasa kati ya makabila yafuatayo: Wabena, Wakinga, Wapangwa, Wawanji, Wakisi na Wamanda.
|
|
|
|---|---|
| Arusha | Dar es Salaam | Dodoma | Geita | Iringa | Kagera | Katavi | Kigoma | Kilimanjaro | Lindi | Manyara | Mara | Mbeya | Morogoro | Mtwara | Mwanza | Njombe | Pemba Kaskazini | Pemba Kusini | Pwani | Rukwa | Ruvuma | Shinyanga | Simiyu | Singida | Tabora | Tanga | Unguja Kaskazini | Unguja Kusini | Unguja Mjini Magharibi | |