Methani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Molekuli ya methani yenye atomi 4 za hidrojeni na atomi 1 ya kaboni

Methani ni kampaundi ya kikemia katika kundi la hidrokaboni yenye fomula CH4 maanake molekuli yake ina atomi 1 ya kaboni na atomi 4 za hidrojeni. Huhesabiwa kati ya alkani ikiwa ni sehemu kubwa ya mchanganyiko wa kawaida ya gesi asilia. Kwa halijoto ya kawaida duniani inatokea kwa umbo la gesi isiyo na herufi wala rangi. Ina nishati nyingi ndani yake inayotumiwa kwa njia ya mitambo. Asili yake iko katika mchakato wa kuoza kwa mimea na dutu ogania kwa hiyo ni fueli kisukuu.

Methani hutazamiwa kati ya gesi za kupandisha halijoto duniani kali zaidi kuliko dioksidi kabonia. Kiwango chake katika angahewa kimezidi upanda tangu upimaji ulianza.

Matumizi[hariri | hariri chanzo]

Methani inawaka haraka kwa hiyo hutumiwa katika maabara kama chanzo cha joto. Katika viwanda vya kutengeneza umeme huchomwa kwa kusudi la kuendesha rafadha za umeme. Katika miji mikubwa hupelekwa kwa mabomba hadi nyumba za watu kwa upishi na kupasha moto nyumba.

Katika miaka ya nyuma kulikuwa pia na majaribio ya kuitumia kama fuele ya kuendesha magari.

Kwa kusudi la kuisafirisha na kuitunza mara nyingi inapashwa baridi na kutunzwa kama kiowevu katika vyupa imara vya feleji au tenki kubwa. Katika hali ya kiowevu inachukua nafasi ndogo tu kuliko gesi.

Uzalishaji[hariri | hariri chanzo]

Methani hupatikana kwa mbinu mbalimbali za kikemia lakini wka kawaida inatokea wakati wa kuchemsha petroliamu katika kiwanda cha kusafisha mafuta.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]