Maksimo Muungamadini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Maximus the Confessor)
Picha takatifu ya Mt. Maksimo kadiri ya mtindo wa Ukristo wa mashariki.
Picha takatifu ya Mt. Maksimo kadiri ya mtindo wa Ukristo wa mashariki.

Maksimo Muungamadini (alizaliwa mwaka 580 akafariki Schemaris, Lazica, leo nchini Georgia, mwaka 662) alikuwa mmonaki padri maarufu kwa teolojia yake.

Miaka 615-645 aliishi Karthago, leo nchini Tunisia.

Jina la pili aliongezewa kutokana na mateso yaliyompata kwa ajili ya imani sahihi: alikatwa mkono wa kulia na ulimi asiweze kuendelea kuitetea wala kwa maandishi wala kwa sauti.

Mtaguso wa tatu wa Konstantinopoli ulimpa ushindi baada ya kifo chake.

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki, Waorthodoksi na wengineo kama mtakatifu na babu wa Kanisa.

Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 13 Agosti[1] au 21 Januari.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Vita ac certamen S. Maximi (PL 90,67-110): Wasifu rasmi kwa Kilatini.
  • P. Sherwood, St Maximus the Confessor. London, 1955
  • Jean-Claude Larchet, Saint Maxime Le Confesseur. Paris, 2003

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.