Martha wa Bethania

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kristo nyumbani mwa Martha na Maria kadiri ya mchoro wa Johannes Vermeer (1654 hivi) unaotunzwa kwenye National Gallery of Scotland, Edinburgh. Martha amesimama karibu na Yesu.
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Martha wa Bethania (jina lake kwa Kiebrania na Kiaramu ni מַרְתָּא, Martâ, kwa Kigiriki Μαρθα, Martha) alikuwa mwanamke wa Bethania, kitongoji cha Yerusalemu, katika karne ya 1[1].

Ndugu zake walikuwa Maria na Lazaro wa Bethania, ambao wote Yesu alifurahia urafiki wao alipokuwa akihiji kwenda Yerusalemu.

Wanaheshimiwa na Wakristo wengi kama watakatifu[2].

Sikukuu yao inaadhimishwa pamoja tarehe 29 Julai[3] au 4 Juni, kadiri ya madhehebu.

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Anajulikana hasa kutokana na Injili, kwa namna ya pekee Injili ya Luka (10:38-42) na Injili ya Yohane (11), katika Agano Jipya ndani ya Biblia ya Kikristo.

Humo anaonekana mwenye silika ya utendaji na imani kwa Yesu Kristo, ambaye alipendezwa na ukarimu wake, pamoja na kumuonya azingatie kwanza kilicho muhimu pekee, yaani kusikiliza Neno la Mungu.

Kisha kumkiri Yesu kuwa Kristo, Mwana wa Mungu aliyekuja ulimwenguni, alishuhudia alivyomfufua kaka yake Lazaro siku nne baada ya kifo chake.

Maneno yake kwa Yesu yalikuwa haya: "Bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa. Lakini hata sasa najua ya kuwa yoyote utakayomwomba Mungu, Mungu atakupa... Naam, Bwana, mimi nimesadiki ya kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni". (Yoh. 11:21-22, 27)

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Martha wa Bethania kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.