Maria Magdalena

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha takatifu ya Waorthodoksi inayomuonyesha Maria Magdalena akibeba manemane kwa ajili ya kupaka upya maiti ya Yesu.
Maria Magdalena chini ya msalaba, akimlilia Kristo aliyekufa.
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Maria Magdalena akiwa amepiga magoti katika kundi la sanamu maarufu kama Stabat Mater; ni kazi ya Gabriel Wuger, 1868.
Maria akiambiwa na mfufuka Noli me Tangere (yaani "Usinishike"); mchoro wa Hans Holbein the Younger, 1524.
Yesu na Maria Magdalena (Noli me tangere). walivyochongwa katika karne ya 13.
Maria Magdalena alivyochorwa na Ary Scheffer huku akifanya malipizi kadiri ya mtazamo wa karne ya 19.
Maria kadiri ya Gheorghe Tattarescu.

Maria Magdalena, yaani wa Magdala (kwa Kigiriki: Μαρία ἡ Μαγδαληνή) ni mmoja kati ya wanafunzi maarufu zaidi wa Yesu wa Nazareti, hasa kutokana na sifa yake ya kuwa mtu wa kwanza kumuona amefufuka (Mk 16:9[1]; Yoh 20:16).

Kwa kuwa alitumwa naye kuwapasha habari hiyo Mitume, kuanzia Thoma wa Akwino anaitwa "Mtume wa Mitume"[2].

Maria wa Magdala kwenye kaburi tupu anavyoonekana katika dirisha la kanisa la Walutheri la St. Matthew huko Charleston, South Carolina, Marekani.
Maria Magdalena alivyochorwa na Anthony Frederick Augustus Sandys, 1860 hivi.

Habari zake kadiri ya Injili[hariri | hariri chanzo]

Ni kwamba, kadiri ya Injili, baada ya kushuhudia kifo cha Yesu na mazishi yake (Mk 15:40-16:1; Math 27:56-28:1; Yoh 19:25), upendo na juhudi vilimfanya mwanamke huyo awahi kwenye kaburi lake alfajiri ya siku ya Jumapili. Huko alitokewa na malaika na kuambiwa amefufuka.

Ndiye aliyewapasha habari hiyo mitume wa Yesu kabla hawajaenda kaburini na kulikuta halina maiti.

Baada ya Maria, hao pia walitokewa na Yesu mwenyewe, kuanzia mtume Petro.

Kabla hajaanza kumfuata, Maria alikuwa amepagawa na mapepo saba (Mk 16:9). Alipoponywa na Yesu, alijitolea kumhudumia na mali yake pamoja na wanawake wengine (Lk 8:2).

Habari yake kuu katika Yoh 20[hariri | hariri chanzo]

1 Alfajiri na mapema Jumapili, kukiwa bado na giza, Maria Magdalene alikwenda kaburini, akaliona lile jiwe limeondolewa mlangoni pa kaburi.

2 Basi, akaenda mbio hadi kwa Petro na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, "Wamemwondoa Bwana kaburini, na wala hatujui walikomweka."

3 Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine wakaenda kaburini.

4 Wote wawili walikimbia lakini yule mwanafunzi mwingine alikimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.

5 Alipoinama na kuchungulia ndani, aliona sanda, lakini hakuingia ndani.

6 Simoni Petro naye akaja akimfuata, akaingia kaburini; humo akaona sanda,

7 na kile kitambaa alichofungwa Yesu kichwani. Hicho kitambaa hakikuwekwa pamoja na hiyo sanda, bali kilikuwa kimekunjwa na kuwekwa mahali peke yake.

8 Kisha yule mwanafunzi mwingine aliyemtangulia kufika kaburini, akaingia pia ndani, akaona, akaaamini.

9 Walikuwa bado hawajaelewa Maandiko Matakatifu yaliyosema kwamba ilikuwa lazima afufuke kutoka wafu).

10 Basi, hao wanafunzi wakarudi nyumbani.

11 Maria alikuwa amesimama nje ya kaburi, akilia. Huku akiwa bado analia, aliinama na kuchungulia kaburini,

12 akawaona malaika wawili waliovaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja kichwani na wa pili miguuni.

13 Hao malaika wakamwuliza, "Mama, kwa nini unalia?" Naye akawaambia, "Wamemwondoa Bwana wangu, na wala sijui walikomweka!"

14 Baada ya kusema hayo, aligeuka nyuma, akamwona Yesu amesimama hapo, lakini asitambue ya kuwa ni Yesu.

15 Yesu akamwuliza, "Mama, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?" Maria, akidhani kwamba huyo ni mtunza bustani, akamwambia, "Mheshimiwa, kama ni wewe umemwondoa, niambie ulikomweka, nami nitamchukua."

16 Yesu akamwambia, "Maria!" Naye Maria akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, "Raboni" (yaani "Mwalimu").

17 Yesu akamwambia, "Usinishike; sijakwenda bado juu kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu uwaambie: nakwenda juu kwa Baba yangu na Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu."

18 Hivyo Maria Magdalene akaenda akawapa habari wale wanafunzi kuwa amemwona Bwana, na kwamba alikuwa amemwambia hivyo.

Heshima aliyopewa baada ya kufa[hariri | hariri chanzo]

Maria Magdalena anahesabiwa mtakatifu katika madhehebu mengi ya Ukristo, akiadhimishwa tarehe 22 Julai[3]. Katika Kanisa la Kilatini Papa Fransisko ameipa hadhi ya sikukuu.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Yesu alipofufuka mapema Jumapili, alijionyesha kwanza kwa Maria Magdalene, ambaye Yesu alikuwa amemtoa pepo saba.
  2. https://www.santiebeati.it/dettaglio/23600
  3. Martyrologium Romanum

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Sanamu yake iliyotengenezwa na Donatello; iko Museo dell'Opera del Duomo, Florence, Italia.
  • Acocella, Joan. "The Saintly Sinner: The Two-Thousand-Year Obsession with Mary Magdalene." The New Yorker, 13 and 20 Februari 2006, p. 140–49. Prompted by controversy surrounding Dan Brown's The Da Vinci Code.
  • Brock, Ann Graham. Mary Magdalene, The First Apostle: The Struggle for Authority. Cambridge, Massachusetts: Harvard University Press, 2003. ISBN 0-674-00966-5. Discusses issues of apostolic authority in the gospels and the Gospel of Peter the competition between Peter and Mary, especially in chapter 7, "The Replacement of Mary Magdalene: A Strategy for Eliminating the Competition."
  • Burstein, Dan, and Arne J. De Keijzer. Secrets of Mary Magdalene. New York: CDS Books, 2006. ISBN 1-59315-205-1.
  • Jansen, Katherine Ludwig. The Making of the Magdalen: Preaching and Popular Devotion in the Later Middle Ages. Princeton, N.J.: Princeton University Press, 2000. ISBN 0-691-05850-4.
  • Kripal, Jeffrey John. (2007), The Serpent's Gift: Gnostic Reflections on the Study of Religion, Chicago: The University of Chicago Press, ISBN 0226453804  ISBN 0-226-45381-2.
  • Pearson, Birger A. "Did Jesus Marry?." Bible Review, Spring 2005, pp 32–39 & 47. Discussion of complete texts.
  • Picknett, Lynn, and Clive Prince. The Templar Revelation. New York: Simon & Schuster, 1997. ISBN 0-593-03870-3. Presents a hypothesis that Mary Magdalene was a priestess who was Jesus' partner in a sacred marriage.
  • Shoemaker, Stephen J. "Rethinking the ‘Gnostic Mary’: Mary of Nazareth and Mary of Magdala in Early Christian Tradition." in Journal of Early Christian Studies, 9 (2001) pp 555–595.
  • Thiering, Barbara. Jesus the Man: Decoding the Real Story of Jesus and Mary Magdalene. New York: Simon & Schulster (Atria Books), 2006. ISBN 1-4165-4138-1.
  • Wellborn, Amy. De-coding Mary Magdalene: Truth, Legend, and Lies. Huntington, Indiana: Our Sunday Visitor, 2006. ISBN 1-59276-209-3. A straightforward accounting of what is well-known of Mary Magdalene.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Maria Magdalena kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.