Makeni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mahali pa Makeni katika Sierra Leone

Makeni ni mji nchini Sierra Leone na makao makuu ya Mkoa wa Kaskazini pia penye utawala wa wilaya ya Bombali. Makeni iko takriban km 120 kaskazini kwa mji mkuu Freetown.

Idadi ya wakazi ni takriban watu 94,000 (kadirio 2007). Mji ulijulikana nchini kwa sababu ya soko lake na msikiti mkubwa. Katika vita ya wenyewe kwa wenyewe ya Sierra Leone uliathiriwa vibaya na kuona uharibifu wa nyumba nyingi. Wanamgambo wa upinzani walikuwa na makao makuu yao mjini hapo.

Rais Ernest Bai Koroma alizaliwa mjini.