Majadiliano ya mtumiaji:ChriKo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta

Hongera ya makala ya Uholanzi. Kuna msaada mmoja: sanduku la habari za nchi - njia rahisi ni kuinakili kutoka en.wikipedia (nakili katika hali ya "edit" ) na kuibandika tu kwa sw.wiki. Halafu ukibonyeza "Mandhari ya mabadilisho" utaona ya kwamba sehemu kubwa ni Kiswahili tayari. Unatafsiri maneno machache tu. Matt ameandaa templeti hii, mimi naona ni msaada mkubwa - --Kipala 19:20, 25 May 2006 (UTC)

Kweli, ni rahisi sana. ChriKo 12:53, 26 May 2006 (UTC)

Yaliyomo

[hariri] Hongera kwa makala ya yule ndege ( Muddyb Blast )

Kimtazamo unaonekana umezama sana kiwikipedia, mimi binafsi nimependezewa sana ile Template ulioitumia kwenye makala ya kuelezea majopu ya ndege, ni mda mrefu sana nilikuwa nikiona zile Template kwenye wikipdeia ya kingereza lakini nikijaribu kunakili zile Template zinakuwa lemavu yaani hazina uwezo kuonekana katika sw.wiki hivyo juhudi zangu zikagonga mwamba kwa upande wa zile Template nikawa nasubiria siku nimfahamishe bwana kipala kuhusiana na ile Template kwa bahti nzuri nikiwa naangalia zile kurasa mpya katika Special Pages nikaona kurasa yako inayohusu ndege hivyo mpango wangu utafanikiwa Hongrea bwana chriko na kila lakheri katika maisha yako huko uliko Ahksante.

--Muddyb Producer 07:09, 6 Septemba 2007 (UTC)Muddyb Blast Producer

[hariri] Aksante Bwana ChriKo

Habari yako ndugu ChriKo, natumai humzima wa afya pole nakazi. kwanza ahsante kwa jibu la haraka ulionigea kuhusiana na ile Template nilkuwa na mpango wa kujaribu tena nikishindwa nitamtafuta ndugu marco kwa msaada zaidi, hata hivyo nilijitahidi mpaka kuiona zile html zake na kujaribu kuhariri baadhi yake ikakubali baadhi zikakataa na pia nashukuru kwa jibu lako la haraka kazi njema na tuendelee hivi hivi kuchangia Wikipedia. --Muddyb Producer 11:06, 7 Septemba 2007 (UTC)Muddyb Blast Producer

[hariri] Okapi

Nimetunga makala nilipoona habari za BBC [[1]]. Naomba uangelie jinsi nilivyojaza sanduku ya uainishaji kama ni sawa. --Kipala 15:17, 10 Juni 2006 (UTC)

[hariri] Mwarobaini

Salaam, nimejaribu kutunga sanduku la uainishaji kwa makala ya Mwarobaini - naomba uangalie na kusahihisha. --Kipala 13:18, 25 Juni 2006 (UTC) Ukipata nafasi - naomba angalia pia Biolojia; nilikuwa nimechoka mito na miji halafu ilikuwa kama pengo kwenye ukurasa wa Mwanzo. --Kipala 16:14, 25 Juni 2006 (UTC) (Pole, nimesafiri, niko Senegal sasa. Nikirudi nitaangalia kurasa hizi. ChriKo 13:00, 30 Juni 2006 (UTC))

Nimesahau kusema: Asante! --Kipala 20:00, 13 Julai 2006 (UTC)

[hariri] Congratutalions, and some questions

Hi ChriKo. I hope you understand English. Congratulations with the 1000 articles in Swahili! It's just great! It's probably the first encyclopedia in an original African language with more than 1000 articles, or?

I have been involved in Wikipedias in several other African languages, such as Bambara. I will be speaking about the Wikipedias I have been involved in. And I would be grateful if you could answer some questions. Also, any other remarks are welcome.

1. Where are you from? Where did you learn Swahili?

2. When did you hear about Wikipedia? And when about the Swahili Wikipedia? When did you start to contribute?

3. What do you think about the future of this project?

thanks, Guaka 20:37, 3 Agosti 2006 (UTC)

Hi Guaka, thanks for the congrats, which I will have to share with the other regular contributors. It's indeed wonderful that the Swahili Wikipedia has breached the 1000 mark. It could well be the first in an African language, I have not checked. Reading your questions, I am again reminded that it is high time I introduced myself on the various Wikipedias to which I contribute. My answers to your questions are a start:
1. I was born in the Netherlands like yourself but left the country after my studies at Wageningen University in 1979. I have been back only occasionally since then. I learned Swahili in Kenya during a study period in 1976/7. Later, I have lived and worked in that country twice for a total of more than 10 years. I have regularly visited Tanzania as well. In addition, I have lived in Niger, Nigeria and Sudan, and travelled extensively throughout the continent. Though I now work in Benin, my Kenyan wife still lives in the highland town of Nanyuki where I visit her twice a year.
2. I learned about Wikipedia in 2004 and it did not take me long to discover the Swahili one. I started to contribute last year.
3. I assume that with "this project" you mean the Swahili Wikipedia. I have to admit that initially I was a bit pessimistic about the future of the project, especially since I had the impression that few native Africans contributed. It was partly the reason for me to start contributing. I am now more optimistic, though cautiously so. I think we need many more Africans to contribute. ChriKo 22:27, 7 Agosti 2006 (UTC)
1) I'm from the UK. I lived in Kenya for six few years when I was growing up, and still manage to visit East Africa about once a year. I picked up a little Swahili when I lived in Kenya, but I've been trying to learn properly for the last couple of years. My Swahili isn't anywhere near good enough to write fresh articles, but I've got a fair bit of experience with MediaWiki and Wikipedia, and when I have time I try and help out here with more technical wiki aspects like templates, categories, translating the user interface etc.
2) I got involved in the English Wikipedia in March 2004, and the Swahili Wikipedia from 2005. I probably first heard about it from the Swahili article in en:.
3) It's very encouraging to have reached 1,000 articles. For a long time it was stuck with around a dozen actual articles of mediocre quality. We really need to have more African Swahili speakers involved with the project, but that may be a matter of waiting for more people to get online and to get faster connections. A Wikipedia edition needs a community of editors actively working and maintaining the project, but for that, a contributor needs a fairly decent connection to the Internet. Matt Crypto 17:35, 8 Agosti 2006 (UTC)
Thats some interesting contributions here, I just came across them today (because I spent August once more in EAK and EAT and did not check very often). I have also had my thoughts about the African share among the authors. At the monent Ndesanjo looks a bit alone holding up the African flag in this wikipedia from the other side of the Atlantic, although he seems to be a tough guy and won´t be scared by all the wazungu invading here. On the other hand we probably have similar motivations for contributing here.
Surely it makes a difference if its all Africans contributing or if most contributions come from "guest-workers". Especially with articles on history, culture and society. A critical mind may call for some "decolonizing of the sw-wiki-mind" after some time from now.
On the other hand I think that it is not so grave with this open concept of wikipedia. Once an encyclopedia worthwhile to be called so is in place it will be used. And it is open to everybody to change and correct. So whatever "harm" I may do with my contributions - it's open for change.
I really find this much more worthwhile than a wikipedia say in English - German - French because this may be the only chance in a nearer future for Kiswahili to have an encyclopedia -I dont see it coming in print from any East African publisher. So lets go. Pecca fortiter! (thats Martin Luther about necessary sins ...) --Kipala 20:48, 13 Septemba 2006 (UTC)

[hariri] Areas of habitat

ChriKo, could it be possible to mention countries and places where the species you describe occur? Would be helpful for interlinking. Just an idea, what do you think? --Kipala 20:48, 13 Septemba 2006 (UTC)

Hi Kipala, welcome back! Yes, countries and places will have to be mentioned when I get down to describing species. For the moment, I am listing groups that have single Swahili names, and providing short descriptions. Describing the individual species will be a lot of work, which I do not have much of at the moment. As a matter of fact, I am thinking of requesting the help of my friends of the Nature Kenya bird group. I may also contact some Tanzanian birders. ChriKo 21:32, 13 Septemba 2006 (UTC)

[hariri] Nahitajii jina

Chriko, naomba nisaidie jina la "Goshawk" (kijer. Habicht). Naiihitaji kwa makala ya Azori. Jina ni lile la ndege. Naweka kwa sasa "tai" lakini si yenyewe. Ukijua naomba sahihisha neno lile moja tu. --Kipala 23:59, 15 Septemba 2006 (UTC)

Jina la "goshawk" ni "kipanga". Nimekwisha kuhariri makala yako. ChriKo 18:41, 16 Septemba 2006 (UTC)


[hariri] mpungate (kakati)??

Chriko, naomba tena msaada ikiwezekana. Nahitaji neno la "cactus" - angalia makala ya "Nembo ya Mexiko". Nimetumia neno "mpungate (kakati)" lakini sina uhakika kama ni sahihi. Ukijua nashukuru ukisahisha. --Kipala 16:34, 27 Septemba 2006 (UTC)

Salamu Kipala. Mpungate ni sawa. "Cacti" haitokei Afrika kwa asili. Spishi chache zimeingizwa na ile iliyotapakaa ni "prickly pear" au mpungate. Ni spishi hii inayoonyeshwa kwa nembo ya Mexiko. ChriKo 10:35, 1 Oktoba 2006 (UTC)

[hariri] Problem of lines inside taxoboxes

Chriko, youa sked me about a problem with line getting into taxoboxes. Does it persist? It could be something with the settings on your screen. I have seen it, too, but it is not consistent and sometimes off again. --Kipala 18:57, 8 Oktoba 2006 (UTC)

[hariri] Majina za nchi

ChriKo, asante kwa ushauri wako kwenye ukurasa wa majidiliano / Afrika. Ushauri wangu ni tofauti kidogo: tusivutane mno kuhusu tahijia ya maneno au kutumia majina namna gani. Tutapoteza muda wetu tu.Tuongeze maumbo mengine kwa kuongeza makala za "Redirect".
Sababu zangu
  • hali halisi hakuna orodha ya majina inayokubaliwa. Hatuna budi kuendelea na maumbo mbalimbali lakini tuweke viungo! Tujitahadhari tukibadilisha kitu ili tusiharibu viungo vilivyopo!
  • orodha za TUKI na BAKITA ya majina ya nchi haifuatwi mara nyingi wala Tanzania wala Kenya. Jinsi inavyoonekana kwangu sehemu yake ni kazi bure. Kama orodha ya Kamusi Hai ni sawa zote mbili hazikubaliani kati yao.
  • Nimejipatia "Atlasi kwa Shule za Msingi Tanzania" (ISBN 9976950403, chapa ya tatu 2005) ambayo ni Atlasi ya pekee kwa Kiswahili ninayofahamu. Haifuati orodha ya TUKI. Lakini hii ni namna ya majina ambayo wanafunzi wanafundishwa nchini Tanzania.
  • inaonekana kuna nchi yenye majina ya pekee kwa Kiswahili yenye uzoefu ya miaka mingi (kwa mfano Misri, Uingereza, Marekani, Shelisheli). Haya tutetee.
    • Nchi nyingine ina majina ya kimapokeo (kama vile Uhabeshi, Uajemi) lakini kuna matumizi sawasawa ya majina ya kimataifa kama vile Ethiopia na Iran. Hatuna budi kuonyesha yote.
    • Kuna nchi nyingine ambazo hazijadiliwi mara nyingi kwa Kiswahili. Hapo matatizo yanaonekana ya orodha zilizotungwa kwenye deski ya TUKI au BAKITA lakini hazitumiki au hutumiwa mara chache sana lakini majina ya kimataifa hutumiwa zaidi. Mifano ni Guinea, Cote d'Ivoire, Nigeria (TUKI: Gini, Kodivaa, Nijeria) na mengi mengine. Nashauri tuongeze Redirect na kuongeza kwa mabano majina haya katika makala ya nchi.
  • Mtindo wa TUKI na BAKITA mara nyingi ni kufuata matamshi ya Kiingereza. Ila tu si rahisi kuelewana kwa sababu katika Kiingereza kuna tofauti katika matamshi (Kiingereza ya kisiwani au ya Marekani auya wapi..). Wameanza tu kwa orodha ya majina machache ya nchi. Baada ya kuandika makala mengi ya nchi naona matata katika mtindo huo. Pamoja na sababu nilizotaja hapo juu inaongeza ugumu wa kuoandika makala upande wa historia, kwa mfano ukieleza asili ya jina la nchi (etimolojia). Kwa mfano Guyana ilipatikana kama jina la koloni tatu za Uingereza, Ufaransa na Uholanzi katika Amerika ya Kusini. Kwa nini tuandike nchi moja "Guyana" lakini nchi nyingine "Gwiyana" (TUKI)?? Kwa nini San Marino iwe "Samarino"?? Hizi ni fikra tupu za deski lakini si matumizi ya lugha.
Nitaandika makala kuhusu tatizo na kutoa orodha ya majina ya nchi kandokando. Nimeshandaa orodha ya TUKI/BAKITA kwa bara na nitaongeza umbo la Atlasi kwa Shule za Msingi.
Naona heri tufuate umbo la Atlasi kwa sababu hii ni kitabu kinachotumiwa, tofauti na orodha zile zilizotajwa. Unaonaje ? --Kipala 18:32, 8 Oktoba 2006 (UTC)
Kipala, nimefahamu sababu zako za kupea nchi majina fulani. Lakini nafikiri si mzuri kutumia kitabu kimoja ili kuchagua majina haya. Ni kweli kama wanaisimu hawakubali kuhusu utumiaji wa majina ya nchi. Hata mimi sipendi majina kadhaa, kama Gine na Kotivaa (hata Samarino). Wala sipendi mtindo wa kufuata matamshi ya Kiingereza. Lakini nani atachagua? Ni sisi wazungu au wazungumzaji wa kienyeji? Inaonekana kwangu kama ni lazima tuhakikishe utumiaji wa majina ya nchi miongoni mwa wananchi na kwa magazeti.
Tusipotumia majina ambayo yanafuata matamshi ya Kiingereza, tutafuata matamshi gani? Kama hakuna jina ambalo linatumika sana, labda tungetumia jina rasmi linalotumika nchini, k.m. Guyana au San Marino. Pengine tunaweza kufuata majina yanayotumika kwa lugha zingine za Bantu. K.m., “Kameruni” hutumika kwa Kinyarwanda. Nafikiri afadhali tutie –i nyuma ya majina rasmi ambayo mwisho yao ni konsonanti, kwa sababu hii haipatikani kwa maneno ya lugha za Bantu.
Kwa kila hali haya ni majadiliano baina ya wazungu wawili. Afadhali tukaribishe wananchi. ChriKo 21:34, 9 Oktoba 2006 (UTC)

[hariri] Karibu tena!

ChriKo, nimefurahi kuona bata yako! Niliogopa umepotea lakini umerudi. Karibu tena! --172.173.207.46 06:00, 9 May 2007 (UTC)

Asante! Nimefanya kazi katika Sudan na Senegal. Kupata mtandao kwa nchi hizi ni ngumu isipokuwa mjini kuu.ChriKo 08:32, 9 May 2007 (UTC)

[hariri] Nimefudhu

Salam Nyiingi Nd. ChriKo, Ni baada ya kimya kingi natafakari nyingi zilizonijaa juu ya sanduku za habari. Ni siku hizi nimeamua kuwa naziumba mwenye kisha naomba msaada wa marekebisho kutoka kwa mkab. Hilo ni baada ya wewe ndugu chriKo kunifahamisha hivyo nimefaulu ahsante. ---Muddyb Blast Producer 05:44, 22 Oktoba 2007 (UTC)

Salamu nyingi ndugu Muddyb. Ninafurahi sana kuona kama umeweza kuandikia wikipedia yetu makala mengi. Kusaidia ni furaha yangu. ChriKo 16:21, 25 Oktoba 2007 (UTC)

[hariri] Uchaguzi

Kuna mapendekezo mapya kwa Wakabidhi na bureaucrat. Naomba angalia ukurasa http://sw.wikipedia.org/wiki/Wikipedia:Wakabidhi --User_talk:Kipala 08:35, 1 Februari 2008 (UTC)

[hariri] Uteuzi mpya

Kuna pendekezo jipya kwa bureaucrat. Naomba uangalie ukurasa wa wakabidhi. --Oliver Stegen 09:16, 1 Machi 2008 (UTC)

[hariri] Sooty Chat

ChriKo, salam. Ndugu ChriKo, unaweza kunieleza mawili matatu kuhusiana na Sooty Chat? Ikiwezekana umwandikie hata makala inayomhusu huyu ndege! Natumai nitakubaliwa ombi langu!! Ubarikiwe.--Mwanaharakati (majadiliano) 07:43, 5 Septemba 2008 (UTC)

Muddyb, salama nyingi. Pole, niko porini. Nitajibu baadaye. ChriKo (majadiliano) 23:41, 11 Septemba 2008 (UTC)
ChriKo, salam. Ahksante kwa ukurasa wa ndege Chati. Lakini labda nikusumbue kidogo (samahani sana). Huyu ndege kweli ni yule, lakini yule niliyemtaka mimi ni yule anayesemekana kuwa yeye anaimba (songbird), ambaye makala yake waweza kuifikia kwa kutumia ukurasa huu! Natumai umenipata, basi ukipata muda tena, naomba ujaribu!! Kazi njema.--Mwanaharakati (Longa) 06:09, 24 Septemba 2008 (UTC)
Salaaam! Sijui kwa Kiswahili anaitwaje. Ila nimeona katika Wikipedia kwa Kiingereza wakimwita Sooty Chat! Ila kwa Kiswahili sijui. Lakini ni Sooty Chat. Kila lakheri...--Mwanaharakati (Longa) 09:05, 26 Septemba 2008 (UTC)
ChriKo, salam. Nashukuru kwa makala nzuri ya ndege mwimbaji!! Pia nakutakia kila lakheri huko uliko, ahsante.--Mwanaharakati (Longa) 05:41, 6 Oktoba 2008 (UTC)

[hariri] Hi ChriKo ;)

Hi! How are you? Could you please help me add a couple of sentences to the Kiswahili version of this interesting article?

Thanks so much! -Ivana Icana (majadiliano) 22:35, 6 Septemba 2008 (UTC)

Hi Ivana, I'll try to find some time. ChriKo (majadiliano) 23:46, 11 Septemba 2008 (UTC)
Salaam, huyu mama ni msumbufu. Angalia majadiliano kwenye ukurasa wa makala. --91.96.107.243 08:33, 12 Septemba 2008 (UTC)
Kweli, nimeona. Asante sana! ChriKo (majadiliano) 20:53, 14 Septemba 2008 (UTC)

[hariri] Familia

ChriKo, salaam. Nafurahia kuona insi unavyoendelea na makala za ndege. Sasa nimegundua jambo. Unaweka Kiungo kwa familia kama kitengo cha uainishaji. Je unaonaje ikibadilishwa kuwa familia (biolojia)? Maana yake neno familia pekee yake itakuwa ni zaidi jumuiya ya kibinadamu. Je, bado inawezakana kubadilisha kiungo hiki? --Kipala (majadiliano) 19:00, 29 Novemba 2008 (UTC)

Salaam, umesema kweli. Nitavibadilisha baadhi kwa kila wakati mmoja. ChriKo (majadiliano) 21:53, 29 Novemba 2008 (UTC)

[hariri] Pole na kazi!

ChriKo,salaaaam! Mzee wangu, nimeona umefanya kazi siyo ya kitoto kiasi hata kustahili kupewa pongezi - HONGERA! Ni baada ya kimya kirefu almanusura tukukatie tamaa kama jinsi ilivyo kwa Nino, Matt, Sj, na wengine weeeengi! Ningependa kusema karibu tena na ninafurahia kuona Waswahili tunazidi kupata makala nyingi za ndege. Na kwa hili, sidhani kama kuna Wikipedia yeyote ya Kiafrika inafikia Wikipedia yetu kwa makala za ndege. Basi tusemaje? Labda hongera zaidi na kila la kheri liwe juu yako! Nikiwa natokea Dar es Salaam, Tanzania, niite Muddyb au--Mwanaharakati (Longa) 08:35, 23 Machi 2009 (UTC)

Muddyb, salaam na asante kwa pongezi zako. Mara kwa mara ninasafiri kwa ajili ya kasi yangu na wakati huu siwezi kuandika makala. Napenda sana kufanya kazi hii na ninafurahi kama kuna watu ambao wanapenda vile ninafanya. Utaona makala mpya nyingi za ndege. ChriKo (majadiliano) 11:30, 24 Machi 2009 (UTC)
Basi tunazikaribisha!!!!!!--Mwanaharakati (Longa) 13:02, 24 Machi 2009 (UTC)

[hariri] 11,000

ChriKo, salaaaaam! Wikipedia yetu imefikisha makala 11,000! Ni furaha iliyoje? Basi tu, niseme tujitahidi kuendeleza na kushauriana kwa kila jambo litakalosaidia Wikipedia yetu kuwa juu! Kila la kheri.--Mwanaharakati (Longa) 15:54, 9 Aprili 2009 (UTC)

Oyeeee!!! Hongera Muddyb, hongera kila mtu aliyechangia. Ninafurahi sana. Nasema tufikishe 20,000 sasa.ChriKo (majadiliano) 21:47, 11 Aprili 2009 (UTC)

[hariri] Swala na wengine

Salaam ChriKo Je unajua kama kuna njia ya kutofautisha kwa Kiswahili kati ya akina swala na wale wanaoitwa "antelope" kwa Kiingereza? --91.62.33.152 11:11, 16 Aprili 2009 (UTC)

Ndiyo, najua. Nitaweka orodha ya spishi katika makala ya swala. Nikipata nafasi nitaandika kurasa za spishi.ChriKo (majadiliano) 12:56, 16 Aprili 2009 (UTC)

[hariri] Mwanaharakati awe bureaucrat

Nimemteua Mwanaharakati achaguliwe kuwa msimamizi mkuu pamoja nasi (b'crat). Naomba upige kura kwenye ukurasa wa wakabidhi. Asante! --Baba Tabita (majadiliano) 07:20, 28 Mei 2009 (UTC)

[hariri] Flowerparty awe mkabidhi

Nimemteua Flowerparty achaguliwe kuwa mkabidhi pamoja nasi. Naomba upige kura kwenye ukurasa wa Wakabidhi. Ahsante! --Mwanaharakati (Longa) 10:36, 9 Julai 2009 (UTC)

[hariri] mradi wa Google kwa ajili ya wikipedia yetu

Bwana ChriKo, salaam!
Nimepata mawasiliano kutoka Christine Moon begin_of_the_skype_highlighting     end_of_the_skype_highlighting huko Palo Alto, California. Yeye anafanya kazi kwa shirika la Google, nao wameanza kupanga mradi au huduma kwa ajili ya wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Tanzania na Kenya ili waelimishwe kuandika makala kwa wikipedia ya Kiswahili. Kumbe!
Christine sasa ametualika kumwandikia maoni yetu, angalia tovuti hiyo:
http://docs.google.com/Doc?docid=0AbIPJ9Nv6udZZGd6MndwcGdfMzFkODNzOG0zYw&hl=en
Bahati mbaya yeye haelewi Kiswahili, kwa hiyo itakuwa lazima kumwandikia kwa Kiingereza. Asante kwa michango yako!
Ni wako katika ujenzi wa lugha yetu, --Baba Tabita (majadiliano) 08:04, 10 Oktoba 2009 (UTC)

Baba Tabita, salamu sana. Ni sawasawa, nitamwandikia nikiwa nimerudi safari yangu. Nipo kusini kwa Senegali sasa. ChriKo (majadiliano) 22:54, 12 Oktoba 2009 (UTC)

[hariri] majadiliano kuhusu utafsiri wa istilahi

Bwana ChriKo, salaam! Nimeanzisha majadiliano mapya kuhusu utafsiri wa istilahi ya wikipedia yetu hapa. Naomba uyaangalie na kuchangia maoni yako. Asante! --Baba Tabita (majadiliano) 09:39, 23 Oktoba 2009 (UTC)

[hariri] Miti

Salaam nafurahia kuona ya kwamba siku hizi umeangalia hata mahali ambako ndege hulala au kutafuta kivuli! --Kipala (majadiliano) 07:31, 10 Desemba 2009 (UTC)

Salaam. Nafurahi kama unapenda vile ninafanya. Nafikiri mimi ni mwanabiolojia wa pekee ambaye anaandikia wikipedia ya Kiswahili makala. Kwa hivyo lazima niandike kuhusu mada yoyote ya biolojia. ChriKo (majadiliano) 21:53, 10 Desemba 2009 (UTC)

[hariri] Hongera ya makala 18,000

Salam, ChriKo! Hongera ya makala 18,000! Kumbe tumefika - japokuwa kuna mengi ya kusahihisha na kufuta pia. Lakini si mbaya tukipongezana! Tuendeleeni jamani.--MwanaharakatiLonga 09:13, 31 Mei 2010 (UTC)

[hariri] Sanduku la uainishaji kwa ng'ombe

Naomba angalia mabadiliko ya sanduku kwa ng'ombe. Nimeongeza elezo kwa Ruminantia na kuweka maelezo yote maandishi madogo. Unaonaje? Ukipenda, tumia - usipopenda - rudisha ukurasa nyuma. (91.98.113.164 21:03, 7 Juni 2010 (UTC)) ni mimi Kipala (majadiliano) 05:32, 8 Juni 2010 (UTC)

Nimeona, asante. Nitaitumia, lakini nimeibadilika vidogo. ChriKo (majadiliano) 16:10, 8 Juni 2010 (UTC)

[hariri] Questionnaire

Nadhani labda wewe umepata pia maswali yale ya Rachel - hapa majibu yangu: Mtumiaji:Kipala/questionnaire - Kipala (majadiliano) 19:07, 30 Juni 2010 (UTC)

[hariri] Jimbo Wales' Wikimania questionnaire

Hi, how are you; I received a message from Jimbo Wales' office, asking if I would like to participate in a questionnaire. As I am not so proficient in Kiswahili, I wonder if you would be interested? /// Hi, mimi nilipokea ujumbe kutoka kwa ofisi ya jimbo Wales ', kuuliza kama napenda kushiriki katika maswali ya. Kama mimi si hivyo magari katika Kiswahili, mimi ajabu kama ingekuwa nia? Kama wewe ni, nami nitawapa ujumbe kwamba una nia. /// Please see: User talk:Mr Accountable#Hello! --Mr Accountable (majadiliano) 18:27, 1 Julai 2010 (UTC)

[hariri] Msaada wa tasfiri

Salam mzee ChriKo. Kumradhi ndugu, unaweza kutoa maoni kwenye ukurusa wa jumuia? Tafadhali tembelea:

Wikipedia:Jumuia#Tafsiri_ya_.22Wikipedia_Usability_Initiative.22_kwa_Kiswahili

Kila la kheri.--MwanaharakatiLonga 13:49, 3 Julai 2010 (UTC)

[hariri] Kura ya kuamua juu ya wakabidhi waliopotea

Karibu kutembelea ukurasa wa wakabidhi na kuamua juu ya wenzetu waliopewa haki za wakabidhi lakini hawakuonekana tangu miezi mingi: Wikipedia:Wakabidhi#Kura_ya_kuondoa_wakabidhi_waliopotea. Tuliwahi kujadili swali hili mwaka uliopita (tazama kwenye ukurasa unaotajwa, juu ya pendekezo) ; sasa njia imeonekana. Kipala (majadiliano) 05:28, 1 Oktoba 2010 (UTC)

[hariri] Chipmunks

Salam, ChriKo! Eti umeona huo ukurasa huo hapo juu? Unaenda katika Wikipedia ya Kiingereza, huruma - sijui hao Chipmunks ni panya au namna gani. Je, unaweza kuumba ukurasa wa Chipmunk japo kwa Kiswahili? Au hata ukielezea namna uonavyo kwa kitaalamu zaidi? Haya, ni hilo ombi langu. Wako Muddyb au,--MwanaharakatiLonga 09:07, 11 Oktoba 2010 (UTC)

Muddyb, salaam. Ndiyo, nimeona ukurasa huo. Chipmunk ni aina ya kindi ambaye anaishi ardhini. Nikipata nafasi ningeweza kuumba ukurasa wa chipmunk, lakini isingekuwa mzuri zaidi niumbe ukurasa wa kindi kwanza? Wako, Christiaan. ChriKo (majadiliano) 13:31, 14 Oktoba 2010 (UTC)
Jamani? Miye sijui lolote kuhusu wanyama! Kwa vile wewe ni mtaalamu wa masuala ya viumbe hai, tafadhali fanya vile ipasavyo! Ikiwa safi, basi nitakuwa mwenye kushukuru. Kila la kheri.--MwanaharakatiLonga 16:55, 14 Oktoba 2010 (UTC)

[hariri] Makala za mamalia

Kipala na Muddyb, salaam. Nawaandikia tena kuhusu rafiki yetu Mjanja. Ameanzisha makala nyingi kuhusu mamalia ambao hawatokei Afrika. Pengine naweza kukubali majina anayotumia, lakini kuna mengine ambayo ameyabuni kabisa au anayatumia kwa njia mbaya. Sidhani ni mzuri kama msemaji asiye mwenyeji anabuni majina mapya. Tafadhali hii ifanywe na wataalamu wa kienyeji. Majina nisiyoyakubali ni yafuatayo:

Mnajua wataalamu (wanazoolojia) ambao watakubali kubuni majina ya wanyama haya kwa Kiswahili? Zamani nimeandikia wanazoolojia katika Tanzania na Kenya, lakini hakuna mtu aliyejibu. ChriKo (majadiliano) 23:02, 20 Julai 2011 (UTC)

Nakubali - asianzishe. Je tufute zote? Menginevyo: nimempata mtaalamu 1 anayejibu mara kadhaa lakiní yeye mwalimu wa astrologia. Wengine: maaraida swa na yako. Kipala (majadiliano) 22:35, 21 Julai 2011 (UTC)
Kwa maoni yangu unaweza kuzifuta. Nitaendelea kutafuta wanazoolojia walio tayari kutafsiri majina ya wanyama wasiotokea Afrika. Itakuwa ngumu kwa sababu siishi katika Afrika ya Mashariki sikuhizi.ChriKo (majadiliano) 23:27, 22 Julai 2011 (UTC)

[hariri] Salaam

ChriKo, nataka kukuambia tu nafurahia kila safari ninapokuona jinsi unavyoendelea kujenga msingi wa wikipedia yetu kazika habari za biolojia. Asante. 91.98.113.164 18:44, 9 Oktoba 2011 (UTC)

Karibu! Furaha ni yangu. (Ulisahau kutia sahihi yako, kwa hivyo sikuweza kukuhutubia kwa jina lako). ChriKo (majadiliano) 20:31, 9 Oktoba 2011 (UTC)

[hariri] Désolé

Hello ChriKo,
I'm afraid I don't speak a single word of swahili, so I could not even read your message of Decembre 4th. If you could have it translated into english, I would be able to read and most probably understand it, and then answer it if needed. Anyway, I thank you very much for the attention you paid to my humble person. Hop [[Utilisateur:Kikuyu3|Kikuyu3]] [[Discussion utilisateur:Kikuyu3|Sous l'Arbre à palabres]] (majadiliano) 20:15, 10 Desemba 2011 (UTC)

Bonjour, Chriko,
Merci de ton intercession sur la page de discussion de l'article "swahili" sur SW:. Ta traduction de ma question a engendré rapidement une réponse d'un contributeur plein de bon sens. J'ai transposé sa réponse sur la page de discussion de l'article. Je viens de faire de même avec ta propre réponse, ainsi nos spécialistes du sujet sauront comment s'orienter.
Asante sana, je crois qu'on dit comme ça. Merci beaucoup et Hop ! [[Utilisateur:Kikuyu3|Kikuyu3]] [[Discussion utilisateur:Kikuyu3|Sous l'Arbre à palabres]] (majadiliano) 11:37, 11 Desemba 2011 (UTC)

[hariri] Bioanuwai

Nisipokosei unatafuta neno "bioanuwai". Ujaribu kuiweka katika google nadhani utaridhika. Wasalaam! 91.98.113.164 11:41, 27 Desemba 2011 (UTC)

Nadhani jibu umepata, mzee wangu. Kama alivyosema ndivyo-iitwavyo!--MwanaharakatiLonga 12:31, 27 Desemba 2011 (UTC)
Asante sana!! ChriKo (majadiliano) 13:42, 27 Desemba 2011 (UTC)

[hariri] Jamii:Mitishamba

Nimekuta leo jamii hii nikashangaa kidogo. Sijaangalia yote lakini ninahisi ni zaidi miti ya matunda ambayo si "mitishamba" - yaani dawa (la kienyeji) kutokana na mimea inayopatikana katika mazingira. Lakini haimaanisha "Miti inayokua shambani". Kama nimekosea naomba maelezo zaidi. Kipala (majadiliano) 13:35, 11 Februari 2012 (UTC)

Ndiyo, uko sahihi. Sikufikiria vizuri. Nikikuta jamii hii, niliangalia ndani yake nikaona miti ya matunda. Kwa hivyo nimeongeza miti ya matunda mingine. Lakini kweli, “mitishamba” ni dawa litokalo shambani au msituni. Nitaondoa miti ya matunda. ChriKo (majadiliano) 19:06, 11 Februari 2012 (UTC)
Vifaa binafsi

Vibadala
Vitendo
Urambazaji
Vifaa