Majadiliano:Zanzibar (Jiji)

Yaliyomo ya ukurasa hayatumiki katika lugha nyingine.
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Jamani naomba usaidizi : nimetunga ukurasa huu ingawa sina uhakika kama jina la makala ni la kweli! Nimefuata mbegu wa makala ambayo nimeikuta ilitumia lugha ya "Jiji la Zanzibar". Nimeendelea nalo lakini sina uhakika kama jina rasmi ni Mji wa Unguja au Mji wa Zanzibar. Tunaye mtu mwenye uhakika (nimeona tu watu huchanganya yote mawili (taz. www.odifpeg.org.uk/publications/greyliterature/fuelwood/masoud/masoud.pdf - mwenyeji anachanganya yote mawili!) --Kipala 01:00, 26 Februari 2006 (UTC)[jibu]

Kumbukumbu yangu na fikra ninazojua mie ni kuwa Zanzibar sio jiji. Halija teuliwa kuwa jiji. Hivi karibuni Tanzania waliteuwa baadhi ya mikoa kuwa jiji: Tanga, Mbeya, Mwanza n.k. Lakini sio zaidi mji minne au mitano ilitajwa kuwa kama ni jiji. Katika orodha hiyo Zanzibar haipo. Ila kama kwa kutaja jiji unaweza kutaja sio mpaka wateuwe iwe jiji. Ni kawaida kwa Kiswahili kutaja jambo kwa kutukuza. Hivyo si vibaya.--Mwanaharakati 11:33, 3 Januari 2008 (UTC)[jibu]