Majadiliano:Uzazi wa mpango

Yaliyomo ya ukurasa hayatumiki katika lugha nyingine.
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Have added some content on birth control translated from English here with references Udhibiti_wa_uzazi. How do people propose merging? James Heilman, MD (talk · contribs · email)(please leave replies on my talk page) 00:34, 30 Novemba 2013 (UTC)[jibu]

Mada imekaa kiupendeleo[hariri chanzo]

Mada hii imekaa kiupendeleo kwani imeandikwa ikiegemea zaidi mtazamo wa kidini bila kujali wapo wasio na dini, pia imekaa katika kuifanya uzazi wa mpango kuonekana jambo baya wakati wikipedia lengo lake ni kumpa taarifa mtu zilizopo bila kuegemea upande wowote, tafadhali ukiandika andika mtazamo wa wahusika wote wanaohusika na jambo unaloliandika. Mfano ungeandika faida na hasara ya kila njia, kisha ni mtu tena aamue afate au asifate, Almasimagorwa (majadiliano) 16:36, 9 Septemba 2016 (UTC)[jibu]

Ndugu, asante kwa maoni yako. Kama unavyosoma hapo juu, kuna ukurasa mwingine juu ya udhibiti wa uzazi ambao unatoa msimamo tofauti, yaani ule unaoenezwa na wale wanaofaidika na biashara ya vifaa vya kuzuia uzazi, ya utoaji mimba na ya maiti za mimba. Acha watu wasikie pia mtazamo wa kutetea uhai, au rekebisha pia ukurasa huo. Kwa vyovyote tusidanganyane kwamba kuharibu mimba ni njia ya kupanga uzazi, kwa sababu mimba ikiwepo uzazi umeshaanza. Kuharibu mimba ni uuaji wa mtu asiye na hatia. Hata kama ni mdogo, ana utambulisho wake wote katika DNA. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 12:37, 10 Septemba 2016 (UTC)[jibu]
Pamoja na hayo, Kiswahili ni lugha ya Kiafrika na watu wetu wana tunu zao ambazo si lazima ziendane na zile za nchi za magharibi. Kwa mfano, nchini Tanzania utoaji mimba ni kosa la jinai kisheria, kama vile ushoga. Lakini wikipedia ya Kiingereza inaegemea kuviunga mkono. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:26, 10 Septemba 2016 (UTC)[jibu]