Ukuta wa Berlin ulitenganisha sehemu mbili za jiji la
Berlin (
Ujerumani) kuanzia
13 Agosti 1961 hadi
9 Novemba 1989. Ukuta huu ulikuwa na urefu wa kilomita 45.3 ukiwa sehemu ya mpaka kati ya madola mawili ya Ujerumani yaliyokuwepo kuanzia
1949 hadi
1990.
Utagulizi: Ugawaji wa Berlin
Chanzo cha ukuta ulikuwa ugawaji wa jiji la Berlin baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia tangu 1945. Nchi washindi ziliamua kugawa Ujerumani yote wakaanzisha kanda nne zilizotawaliwa na Umoja wa Kisovyeti, Marekani, Uingereza na Ufaransa. Berlin ilikuwa ndani ya kanda la kisovyeti lakini ikiwa mji mkuu wa Ujerumani ilitangazwa kuwa mkoa wa pekee ikagawiwa pia katika kanda nne za washindi.
Ujenzi wa ukuta wa Berlin
1961 serikali ya mashariki iliona ni lazima kuzuia wakimbizi wengi kwenda Berlin Magharibi. Hapa walikata shauri ya kutenganisha sehemu mbili za jiji kwa njia ya ukuta na fensi. Walipata kibali cha uongozi wa Umoja wa Kisovyeti wakaandaa akiba za matofali, simiti na waya ya miiba.
Usiku wa tar. 12 kwenda 13 Agosti 1961 wanajeshi na polisi maelfu walitumwa kusimama mpakani mjini Berlin walipoangalia wajenzi walioanza kujenga ukuta na kuziba mpaka ndani ya jiji. Soma zaidi...