Mwanzo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

(Elekezwa kutoka Main Page)
Karibu kwenye Wikipedia,
kamusi elezo huru, kila mtu anaweza kuihariri!
Hadi leo tuna makala takriban 14,661 kwa Kiswahili
     

     

Kamusi Elezo ya Kiswahili

Karibu kwenye Wikipedia ya Kiswahili!

Wikipedia ni mradi wa kuandika kamusi elezo kamili na sahihi ya maandishi huru.

Kila mtu anaweza kuhariri makala yoyote, kutoa makosa ya lugha, kutohoa maneno na kuendeleza na kukuza makala, kwa kuandika kwa ufupi au kwa urefu. Angalia Msaada wa kuanzisha makala ili ujifunze unavyoweza kuhariri au kusanifisha ukurasa. Usisite kushiriki; kwa sababu huu ni mradi wa ushirikiano, na hautaisha kamwe. Kamusi elezo itaimarika vizuri zaidi kila wakati. Angalia ukurasa wa jumuia, ukurasa wa jamii, na ule wa makala za msingi za kamusi elezo ili kung'amua unaweza kufanya kazi zipi ili kuboresha Wikipedia.


Je, wajua...

Kutoka kwenye mkusanyiko wa makala za Wikipedia:

Chansella wa Ujerumani



Makala ya wiki

Ukuta wa Berlin

Ukuta wa Berlin ulitenganisha sehemu mbili za jiji la Berlin (Ujerumani) kuanzia 13 Agosti 1961 hadi 9 Novemba 1989. Ukuta huu ulikuwa na urefu wa kilomita 45.3 ukiwa sehemu ya mpaka kati ya madola mawili ya Ujerumani yaliyokuwepo kuanzia 1949 hadi 1990.

Utagulizi: Ugawaji wa Berlin

Chanzo cha ukuta ulikuwa ugawaji wa jiji la Berlin baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia tangu 1945. Nchi washindi ziliamua kugawa Ujerumani yote wakaanzisha kanda nne zilizotawaliwa na Umoja wa Kisovyeti, Marekani, Uingereza na Ufaransa. Berlin ilikuwa ndani ya kanda la kisovyeti lakini ikiwa mji mkuu wa Ujerumani ilitangazwa kuwa mkoa wa pekee ikagawiwa pia katika kanda nne za washindi.

Ujenzi wa ukuta wa Berlin

1961 serikali ya mashariki iliona ni lazima kuzuia wakimbizi wengi kwenda Berlin Magharibi. Hapa walikata shauri ya kutenganisha sehemu mbili za jiji kwa njia ya ukuta na fensi. Walipata kibali cha uongozi wa Umoja wa Kisovyeti wakaandaa akiba za matofali, simiti na waya ya miiba.

Usiku wa tar. 12 kwenda 13 Agosti 1961 wanajeshi na polisi maelfu walitumwa kusimama mpakani mjini Berlin walipoangalia wajenzi walioanza kujenga ukuta na kuziba mpaka ndani ya jiji. Soma zaidi...

Picha nzuri ya wiki

Tausi

Tausi ni ndege wakubwa wa jenasi Pavo na Afropavo katika familia ya Phasianidae. Dume ana rangi ing’aayo ya majani au buluu na mkia wake ni mrefu mwenye rangi nyingi. Jike ana rangi inayofifia pengine kahawia tu. Jinsia zote zina ushungi. Dume hukoga mkia kwa ubembelezi. Hula matunda, maua, wadudu na watambazi. Hutaga mayai matatu hadi manane ardhini.

Jumuia za Wikimedia

Commons
Ghala ya Nyaraka za Picha na Sauti
Meta-Wiki
Uratibu wa Miradi yote ya Wikimedia
Wiktionary-logo-en.png
Wikamusi
Kamusi na Tesauri
Wikibooks-logo.png
Wikitabu
Vitabu vya bure na Miongozo ya Kufundishia
Wikiquote-logo-51px.png
Wikidondoo
Mkusanyiko wa Nukuu Huria
Wikisource-logo.png
Wikisource
Nyaraka Huru na za Bure
Wikispishi
Kamusi ya Spishi
Wikiversity-logo.png
Wikichuo
Jumuia ya elimu
Wikinews-logo.png
Wikihabari
Habari Huru na Bure