Mageuko ya spishi
Mageuko ya spishi ni nadharia ya kisayansi iliyobuniwa na kutumiwa na wataalamu wa biolojia. Inasema ya kwamba spishi za viumbehai zilizopo duniani leo zimetokana na spishi zilizokuwa tofauti za zamani. Nadharia hii inategemea ya kwamba awali maisha yote yametokana na maumbo asilia. Katika wazo hili spishi zote jinsi zilivyo sasa zinaendelea kubadilika.
Msingi wa nadharia hii ni mabaki ya kisukuku ya viumbehai ambao hawapo tena duniani lakini wanaofanana kiasi na viumbehai wa leo, pamoja na ulinganifu wa spishi za karibu na mbali zaidi. Nadharia ya mageuko ya spishi inalenga kueleza mabadiliko haya.
Mtaalamu Mwingereza Charles Darwin anajulikana kama mfumbuzi wa nadharia hii.
Leo hii ni nadharia ya kibiolojia inayokubaliwa na wataalamu wengi hata kama kuna wapinzani kadhaa hasa upande wa wenye imani kali ya dini, lakini pia wachache kwa sababu za kitaalamu.
Marejeo [hariri]
Viungo vya Nje [hariri]
- Understanding Evolution - a guide prepared by the University of California at Berkeley
- Howstuffworks.com—How Evolution Works
- The Big Picture on Evolution by the Welcome Trust.
- Online collection of Darwin's papers at the University of Cambridge
- Talk Origins in depth website on information about evoluton and the evidence for it
- National Center for Science EducationInformation on how evolution works
- PBS, on evolution site