Mafinga

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mafinga ni mji katika Mkoa wa Iringa, Tanzania. Eneo hili limepata halmashauri yake na hadhi ya mji (town) tangu mwaka 2007.

Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, wilaya ina wakazi wapatao 51,902 waishio humo. [1] Katika sensa ya mwaka 2022 walihesabiwa 122,329 [2].

Mafinga iko kando ya barabara ya TANZAM kutoka Dar es Salaam kwenda Mbeya, Zambia na Malawi.

Wakati wa ukoloni iliitwa "John`s Corner". Kuna sehemu mbili yaani Mafinga yenyewe na kwa umbali wa kilomita 15 iko Sao Hill.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. 2012 Population and housing census, Population Distribution by Administrative Areas (en). National Bureau of Statistics Ministry of Finance Dar es Salaam, Tanzania. Jalada kutoka ya awali juu ya 2013-05-11.
  2. https://www.nbs.go.tz
Kata za Wilaya ya Mafinga - Mkoa wa Iringa - Tanzania

Boma | Bumilayinga | Changarawe | Isalavanu | Kinyanambo | Rungemba | Sao Hill | Upendo | Wambi


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Iringa bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mafinga kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.