Madende

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Madende
Madende madoadoa
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia: Muscicapidae (Ndege walio na mnasaba na shore)
Nusufamilia: Saxicolinae (Ndege wanaofanana na kurumbiza)
Jenasi: Cichladusa
W. Peters, 1863

Madende ni ndege wa jenasi Cichladusa katika familia ya Muscicapidae. Zamani waliainishwa katika familia ya mikesha (Turdidae). Wana mnasaba na kurumbiza na wanafanana nao. Wana rangi ya kahawa mgongoni na nyeupe chini; madende madoadoa ana madoa meusi kidarini na tumboni. Hawa ni ndege wa misitu mikavu ya Afrika. Madume ya spishi hizi waimba vizuri. Hula wadudu hasa. Hujenga tago lao kwa umbo wa kikombe katika au chini ya kichaka. Jike huyataga mayai 2-4.

[hariri] Spishi

Vifaa binafsi
Maeneo ya wiki

Vibadala
Vitendo
Urambazaji
Vifaa
Lugha zingine