Lugha za Afrika
Lugha za Afrika ni zaidi ya 2000.
Baadhi ya lugha hizi zina wasemaji mamilioni kama vile Kiswahili, Kihausa, Kiigbo, au Kiyoruba. Lugha nyingine zina wasemaji wachache sana hata zinaelekea kupotea.
Vikundi vya lugha[hariri]
Vikundi vikubwa vya lugha za Kiafrika ni hasa:
- Lugha za Kiafrika-Kiasia - lugha 350 zenye wasemaji milioni 350 katika Afrika ya Kaskazini na Asia ya Magharibi, hasa Kiarabu na Kiamhara
- Lugha za Kikongo-Kiniger - lugha 1,400 zenye wasemaji milioni 370 katika Afrika ya Magharibi, mashariki na kusini Hizi ni pamoja na lugha za Kibantu kama Kiswahili.
- Lugha za Kisudani (Nilo-Sahara) - lugha 200 zenye wasemaji milioni 35 kati ya Sudani hadi Mali na Tanzania. Kati yake kuna Kijaluo na Kimaasai.
- Lugha za Khoisan - lugha 28 zenye wasemaji 355,000 katika Afrika ya Kusini na Tanzania. Wataalamu wanaelekea kuziona kuwa ndizo lugha zinazofanana zaidi na ile ya asili ya binadamu. Kati yake ipo lugha ya Wasandawe wa Tanzania.
Kuna pia maeneo penye wasemaji wa lugha zenye asili nje ya Afrika kama vile:
- lugha za Kiaustronesia katika Madagaska
- lugha za Kihindi-Kiulaya hasa katika Afrika ya Kusini halafu kama lugha rasmi kote Afrika kama vile Kiingereza, Kifaransa, Kireno, Kiafrikaans, Kihispania, Kitamil, Kigujarati, Kipunjabi na Kijerumani.
Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.
|
||||||||||||||