Lango:Jiografia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Milango ya Wikipedia: Sanaa · Utamaduni · Jiografia · Afya · Historia · Hisabati · Sayansi · Falsafa · Dini · Jamii · Teknolojia

Lango la Jiografia

Jiografia ni somo la Dunia na vipengele vyake, wakazi wake, na maajabu yake. Neno jiografia linatokana na maneno ya Kigiriki ("Dunia") na graphein ("kuandika"). Ina maana ya "kuandika kuhusu Dunia". Neno hili lilianza kutumiwa na mwanasayansi Eratosthenes (276-194 KK).

Sehemu za jiografia ni vitu kama mabara, bahari, mito na milima. Wakazi wake ni watu wote na wanyama waishio juu yake. Maajabu yake ni vitu vinavyotokea, kama vile maji kujaa na kupwa, upepo, na tetemeko la ardhi.

Mabara

Makala iliyochaguliwa

Mabamba gandunia ya dunia yetu

Bamba gandunia ni kipande kikubwa cha ganda la dunia. Hoja la sayansi kuhusu gandunia ni ya kwamba ganda la dunia limevunjika kwa vipande mbalimbali vinavyoitwa mabamba. Kila bamba lapakana na mabamba mengine. Mabamba yasukumwa na mikondo ya moto chini yao kama majani yanayokaa usoni wa maji inayoanza kuchemka katika sufuria. Hivyo kila bamba lina mwendo wake wa pekee pamoja na au dhidi ya mabamba mengine.

Mabamba haya yote yameonekana kuwa na mwendo wa sentimita kadhaa (2 - 20 cm zimepimwa) kwa mwaka. Mwendo huu husababishwa na nguvu ya magma (mwamba moto wa kiowevu) inayopanda juu na kusukuma mabamba haya.

Je, wajua...?

Vitu unavyoweza kufanya

Masharika ya Wikimedia