Kuki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha ya kuki
Logo ya kuki ya HTTP

Kuki ni tafsiri ya muda[1] ya neno la Kiingereza cookie, ambalo maana yake asili ni biskuti au keki ndogo, lakini katika utarakilishi linatumika ili kompyuta yenye kurasa za tovuti iweze kuwasaliana na watazamaji.

Programu za tovuti hizi zinahifadhi habari kadhaa za mtazamaji au mtumiaji (k.m. jina la mtumiaji, neno la siri, ruhusa, mapendekezo) kwenye kompyuta ya mtazamaji mwenyewe[2]. Hivi mtazamaji anatambuliwa kila wakati anaingia kwenye tovuti hii.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Pendekezo la "kuki" limepelekwa mbele na Mradi wa Kilinux (Linux na Open Office kwa Kiswahili) wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Mradi wa kampuni ya Microsoft ya kuswahilisha programu ya "Windows" umependekeza kutumia neno "kidakuzi" pamoja na "kuki".
  2. What are computer cookies?. Tovuti ya us.norton.com, iliangaliwa Desemba 2021

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]