Samueli II

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Kitabu cha Pili cha Samueli)

Kitabu cha pili cha Samueli kilikuwa sehemu ya pili ya Kitabu cha Samweli katika Tanakh (yaani Biblia ya Kiebrania) kabla hakijagawiwa pande mbili kutokana na ukubwa wake.

Kuanzia tafsiri ya kwanza (ya Kigiriki) inayojulikana kama Septuaginta, halafu katika Agano la Kale la Biblia ya Ukristo, kinahesabiwa kama kitabu kinachojitegemea.

Hata hivyo mada yake na ya Kitabu cha kwanza (Samueli I) ni moja: kueleza habari za mwanzo wa ufalme wa Israeli chini ya Samueli aliyewapaka mafuta awaweke wakfu mfalme Sauli halafu mfalme Daudi.

Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.

Kwa habari zaidi tazama Vitabu vya Samweli.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Vitabu vya Agano la Kale

Mwanzo * Kutoka * Walawi * Hesabu * Kumbukumbu * Yoshua * Waamuzi * Ruthu * Samueli I * Samueli II * Wafalme I * Wafalme II * Mambo ya Nyakati I * Mambo ya Nyakati II * Ezra * Nehemia * TobitiDK * YudithiDK * Esta * Wamakabayo IDK * Wamakabayo IIDK * Yobu * Zaburi * Methali * Mhubiri * Hekima DK * SiraDK * Wimbo Bora * Isaya * Yeremia * Maombolezo * BarukuDK * Ezekieli * Danieli * Hosea * Yoeli * Amosi * Obadia * Yona * Mika * Nahumu * Habakuki * Sefania * Hagai * Zekaria * Malaki

Alama ya DK inaonyesha vitabu vya deuterokanoni visivyopatikana katika matoleo yote ya Biblia.

Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Samueli II kama historia yake au athari wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.