Kinyemba
Kinyemba ni lugha ya Kibantu nchini Angola inayozungumzwa na Wanyemba. Mwaka wa 2001 idadi ya wasemaji wa Kinyemba nchini Angola imehesabiwa kuwa watu 222,000. Pia kuna wasemaji wa Kinyemba nchi za Namibia na Zambia. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kinyemba kiko katika kundi la K20.
Viungo vya nje [hariri]
- lugha ya Kinyemba kwenye Multitree
- ramani ya Kinyemba
- http://www.ethnologue.org/show_language.asp?code=nba
Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.