Kinorwei
| Kinorwei | ||
|---|---|---|
| Norsk | ||
| Pronunciation | [nɔʂk] | |
| Inazungumzwa nchini | Norwei | |
| Jumla ya wazungumzaji | 4,700,000 | |
| Familia ya lugha | Lugha za Kihindi-Kiulaya | |
| Standard forms | ||
| Mfumo wa uandikaji | Alfabeti ya Kilatini | |
| Hadhi rasmi | ||
| Lugha rasmi nchini | Norwei | |
| Hurekebishwa na | Språkrådet | |
| Misimbo ya lugha | ||
| ISO 639-1 | no | |
| ISO 639-2 | nor | |
| ISO 639-3 | nor | |
| Note: This page may contain IPA phonetic symbols in Unicode. | ||
Kinorwei (Kinorwei: norsk) ni lugha ya Kigermanik ya Kaskazini katika jamii ya lugha za Kihindi-Kiulaya.
Kinorwei kinasemwa na watu 4,700,000 hivi, na ni lugha rasmi nchini Norwei.
Kinorwei, Kiswidi na Kidenmark vinavyoitwa lugha za Skandinavia ya bara vinahusiana sana.
Kinorwei kina insha rasmi mbili: bokmål na nynorsk.
Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.