Kimbugwe

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kimbugwe ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania inayozungumzwa na Wambugwe. Mwaka wa 1999 idadi ya wasemaji wa Kimbugwe imehesabiwa kuwa watu 24,000. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kimbugwe iko katika kundi la F30. Lugha ya Kimbugwe inafanana na Kirangi, na Warangi wengi wanadai kwamba Kimbugwe ni lahaja ya Kirangi tu. Kisayansi lakini Kimbugwe ni lugha yenyewe kwa vile asilimia 74 tu za msamiati wake zina chanzo kimoja na Kirangi. Wasemaji wakikutana wanagundua kuwa lugha hizo mbili hazitambulikani moja kwa nyingine bila kujifunza ile nyingine.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Maho, Jouni & Bonny Sands. 2002. The languages of Tanzania: a bibliography. (Orientalia et africana gothoburgensia, no 17.) Göteborg: Acta Universitatis Gothoburgensis. Pp ix, 428. ISBN 91-7346-454-6

Kitabu hiki kinataja marejeo mengine kama:

  • Dempwolff, Otto. 1915/16. Beiträge zur Kenntnis der Sprachen in Deutsch-Ostafrika. Teil 7: Buwe (Mbugwe). Zeitschrift für Kolonialsprachen, 6, uk.1-27.
Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kimbugwe kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.