Kilufu
Kilufu ni lugha ya Kiniger-Kongo nchini Nigeria inayozungumzwa na Walufu. Mwaka wa 2006 idadi ya Walufu imehesabiwa kuwa watu 3200 lakini wengi wao wamebadilisha lugha kuongea Kijukun. Kwa vile hasa ni wazee tu ambao wameendelea kuongea Kilufu inawezekana kwamba Kilufu kitatoweka hivi karibuni. Ingawa uainishaji wa lugha ya Kilufu kwa ndani zaidi haujulikani, imesemekana kuwa ilifanana na lugha ya Kibete ambayo ni katika kundi la Kijukunoidi linalofanana na lugha za Kibantu.
Viungo vya nje [hariri]
- lugha ya Kilufu kwenye Multitree
- ramani ya Kilufu
- http://www.ethnologue.org/show_language.asp?code=ldq
Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.