Jakaya Kikwete

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Kikwete)
Rukia: urambazaji, tafuta
Dk Jakaya Kikwete


Aliingia ofisini 
21 December 2005
Waziri Mkuu Edward Lowassa (2005-08)
Mizengo Pinda
Makamu wa Rais Ali Mohamed Shein (2005-10)
Mohamed Gharib Bilal
mtangulizi Benjamin Mkapa

Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika
Muda wa Utawala
31 January 2008 – 2 February 2009
mtangulizi John Kufuor
aliyemfuata Muammar al-Gaddafi

Muda wa Utawala
November 1995 – 21 December 2005
Rais Benjamin Mkapa
aliyemfuata Asha-Rose Migiro

Muda wa Utawala
1994 – 1995
Rais Ali Hassan Mwinyi
mtangulizi Steven Kibona
aliyemfuata Simon Mbilinyi

Mbunge wa Tanzania
Muda wa Utawala
1990 – 2005
aliyemfuata Ramadhani Maneno
Constituency Bagamoyo (1990-95)
Chalinze (1995-2005)

tarehe ya kuzaliwa 7 Oktoba 1950 (1950-10-07) (umri 62)
Msoga, Tanganyika
utaifa Mtanzania
ndoa Salma Kikwete
watoto 8
makazi 1 Ocean Road,
11400, Dar es Salaam
mhitimu wa UDSM (BA)
Fani yake Mchumi
dini Uislamu
tovuti jakayakikwete.com
Military service
Allegiance Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Service/branch Jeshi la Tanzania
Years of service 1976-1992
Rank Luteni Kanali

Jakaya Mrisho Kikwete tangu tarehe 21 Desemba 2005 ni rais wa nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Jakaya Kikwete pamoja na marais waliostaafu Benjamin Mkapa na Alhaji Ali Hassan Mwinyi

Yaliyomo

Asili [hariri]

Amezaliwa 7 Oktoba 1950 katika kijiji cha Msoga, kata ya Lugoba, tarafa ya Msoga, Jimbo la Chalinze, Wilaya ya Bagamoyo, mkoa wa Pwani. Lugha ya mama ilikuwa Kikwere.

Alizaliwa katika familia ya wanasiasa. Babu yake Mzee Mrisho Kikwete alikuwa chifu wa Wakwere. Baba yake alikuwa Mkuu wa Wilaya Pangani, Same na Tanga. Jakaya Kikwete amesimulia hadithi ya kifamilia ya kuwa wakati mama yake alipokuwa mja mzito naye, Babu alitamka kuwa ikiwa mtoto atakuwa wa kiume atampatia urithi wa cheo chake.

Masomo [hariri]

1958 – 1961 akasoma Shule ya Msingi Msoga, halafu 1962 – 1965 Shule ya Middle School Lusonga, halafu Shule ya Sekondari Kibaha akiongeza A-level huko Shule ya Sekondari Tanga. Kuanzia mwaka 1972 alisoma uchumi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akimaliza digrii yake mwaka 1978. Akajiunga na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Jakaya aliposoma Shule ya Sekondari ya Kibaha alikuwa mwenyekiti wa wanafunzi na pia wa Vijana wa TANU. Shule ya Sekondari Tanga alikuwa Kiranja Mkuu na pia kiongozi wa timu ya mpira. UDS alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa halmashauri ya wanafunzi.

TzJk.jpg

Kupanda ngazi katika siasa [hariri]

1988 akateuliwa kuwa mbunge na waziri msaidizi. 1990 alichaguliwa kuwa mbunge wa Bagamoyo/Chalinze akirudishwa kila uchaguzi hadi mw. 2000. Akawa waziri akipita katika wizara za maji na fedha.

1995 alijaribu kuchaguliwa kuwa mgombea wa uraisi upande wa CCM. Inasemekana ya kwamba Mwl. Julius Nyerere alimwomba wakati ule kumwachia Benjamin Mkapa nafasi aliyeteuliwa na Halmashauri Kuu ya CCM. Kikwete akawa Waziri ya Mambo ya Nje katika serikali zote mbili za Mkapa.

Mwaka 2005 alifaulu kuteuliwa mgombea wa CCM kwa nafasi ya raisi na akashinda uchaguzi wa Desemba 2005 akizoa 80% za kura zote.

Viungo vya nje [hariri]

Bendera ya Tanzania Orodha ya Marais wa Tanzania
Julius NyerereAli Hassan MwinyiBenjamin MkapaJakaya Kikwete