Kiguudau

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kiguudau
Kiguudau wa Afrika
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Gruiformes (Ndege kama makorongo)
Familia: Heliornithidae (Ndege walio na mnasaba na viguudau)
Jenasi: Heliopais G.R. Gray, 1849

Heliornis Bonnaterre, 1791
Podica Lesson, 1831

Viguudau ni ndege wa maji wa familia Heliornithidae. Familia hii ina spishi tatu tu, kila moja katika jenasi yake. Ndege hawa wana mwili mwembamba, shingo refu, mkia mpana na domo lenye ncha kali. Vidole vyao vina ndewe zinazowasaidia kuogelea. Wanatokea kanda za tropiki kwa maji yatiririkayo polepole au katika vinamasi na mabwawa ya mikoko. Hula wadudu, makoa, gegereka, vyura na samaki wadogo. Hujenga tago lao la vitawi na mimea kwa matete.

[hariri] Spishi ya Afrika

[hariri] Spishi za mabara mengine

[hariri] Picha