Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Viguudau ni ndege wa maji wa familia Heliornithidae. Familia hii ina spishi tatu tu, kila moja katika jenasi yake. Ndege hawa wana mwili mwembamba, shingo refu, mkia mpana na domo lenye ncha kali. Vidole vyao vina ndewe zinazowasaidia kuogelea. Wanatokea kanda za tropiki kwa maji yatiririkayo polepole au katika vinamasi na mabwawa ya mikoko. Hula wadudu, makoa, gegereka, vyura na samaki wadogo. Hujenga tago lao la vitawi na mimea kwa matete.
[hariri] Spishi ya Afrika
[hariri] Spishi za mabara mengine