Kicheki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Kiceki)

Kicheki ni lugha ya Kislavoni katika familia ya lugha za Kislavoni cha Magharibi inayotumiwa nchini Ucheki. Pia kuna wasemaji takriban milioni mbili nje ya Ucheki.

Kicheki ni lugha ya karibu na Kislovakia na Kisorbi. Kinaandikwa kwa alfabeti ya Kilatini.

Wageni hushtuka mara nyingi wakiona maneno bila vokali, kwa mfano sentensi "Strč prst skrz krk". Sababu yake ni kwamba herufi za r na l zinaweza kuhesabiwa kama silabi (utaratibu unaofanana na "m" kama mwanzo wa neno mbele ya konsonanti katika lugha za Kibantu: m-fano, M-swahili).

Sarufi inapanga nomino zote katika jinsia tatu.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kicheki kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.