Kanisa la Biblia Tanzania

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kanisa la Biblia Dodoma baada ya ibada ya jumapili

Kanisa la Biblia Tanzania (KLB) ni kanisa dogo la Uprotestanti lenye shirika 90 hasa kusini mwa Tanzania, katika mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma; kuna pia shirika kadhaa katika mikoa ya Dodoma, Dar es Salaam na Kilimanjaro.

Makao makuu yako Mbesa (wilaya ya Tunduru).

Limeandikishwa na serikali kwa namba 5881.

Kanisa la Biblia hufuata mtindo wa Ndugu wa Plymouth, hivyo kila ushirika unajitegemea na kanisa kwa jumla ni ushirikiano wa shirika zake.

Kanisa hili lilianzishwa na wamisionari kutoka Ujerumani; tangu 1959 linaendelea kushirikiana na CMML (Christian Mission in Many Lands) hata kama utawala wa kanisa umo mikononi mwa Watanzania.

Pamoja na kazi ya kiroho KLB huendesha pia miradi ya kijamii kama vile shule, vyuo, hospitali na kituo cha kutunza watoto yatima.

Ubatizo kjijini Mbesa.

Kati ya miradi yake ni

Kuna pia miradi ya kilimo. Kanisa linaanzisha pia shule ya sekondari huko Mtwara.

KLB inatoa kozi ya Biblia kwa njia ya barua (Emmaus Shule ya Biblia) na kushirikiana na Chuo cha Biblia Berea (Moshi).

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]