John Ngugi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rekodi za medali
Faili:Badilisha picha male.svg
John Ngugi
Men's Wanariadha
Anawakilisha nchi Bendera ya Kenya Kenya
Michezo ya Olimpiki
Dhahabu 1988 Seoul 5000 metres
All-Africa Games
Dhahabu 1987 Nairobi 5000 metres

John Ngugi Kamau (alizaliwa 10 Mei 1962 katika sehemu ya Kigumo, wilayani Muranga) ni mkimbimbiaji wa zamani wa Kenya na mara nyingi huitwa mmoja wa wanariadha bora nchini katika mbio za “cross-country” na ni mshindi wa mita 5,000 katika Olimpiki ya mwaka wa 1988.

Ngugi ni mzaliwa wa Kigumo na mafanikio yake ya mapema ya kimataifa yalikuja katika michuano ya dunia Cross Country, ambapo alishinda taji nne mfululizo kati ya mwaka wa 1986 na 1989 (hii ililkuwa rekodi ya uanariadha) na kwa ujumla taji tano.

Ngugi alijiimarisha mwenyewe kama mkimbiaji wa mburuzo yake aliposhinda mbio ya mita 5000 katika Michuano ya Dunia ya mwaka wa 1987 katika mji mkuu wa Roma. Katika fainali, Ngugi alichukua uongozi alipofikia kilomita ya pili, lakini licha ya mbinu zake za uongozi katika mbio hizo, alipitwa na wanariadha wenzake wakati wa kumaliza, na kumaliza katika nafasi kumi na mbili; nafasi ya kusikitisha. Alishinda mbio za mita 5000 katika Michezo ya All-Africa ya mwaka wa 1987 uliofanyika nchini Kenya.

Katika Michezo ya Olimpiki yaliyofanyika katika mji mkuu wa Seoul, Ngugi alichukua uongozi baada ya kilomita moja na akafanikiwa kuchukua uongozi wa mita 50. Ingawa uoongozi wake ulipunguzwa wakati mbio za kasi zilitarajiwa katika Lapu ya mwisho, bado Ngugi aliweza kushinda kwa mita 30.

Wakati Michezo ya Jumuiya ya Madola ya mwaka wa 1990 katika mji mkuu wa Auckland, nchini New Zealand, Ngugi alijaribu kutimia mbinu sawa na zile ambazo zilimsaidia kushinda medali ya dhahabu ya Olimpiki. Ingawa aliteguka na kuanguka baada lapu mbili tu na kupoteza mita 35 kwa washindani wenzake, aliweza kulishika kundi lililokuwa likiongoza na kuimarisha pengo la mita 40 wakati kengele ya lapu ya mwisho iligongwa. Lakini wakati huo, juhudi zake hazikutosha kwani Andrew Lloyd kutoka Australia alishinda na sekunde 0.08 tu katika mmalizio wa ajabu.

Ngugu alirejea mwaka wa 1992 kulikamata taji la dunia la Cross Country kwa mara ya tano.

Ngugu alirejea mwaka wa 1992 kulikamata taji la dunia la Cross Country kwa mara ya tano. Mwaka wa 1993 Ngugi alikataa kufanyiwa jaribio la dawa la nje-ya-ushindani [9] na awali alipokea marufuku ya miaka minne lakini baadaye ilipunguzwa kwa miaka miwili kutokana na 'hali za ajabu'. Kwa ufanisi huu ulikamilisha wasifu wake kama mwanariadha.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]