Jini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Imam Ali akiteka Jinn, Ahsan-ol-Kobar (1568) Golestan Palace

Jini ni jina la Kiswahili lililotokana na neno la Kiarabu الجن‎, al-jinn.

Majini ni viumbe wanaosadikika kuishi katika mazingira ya kila aina; pia baadhi ya watu wanaamini majini ni viumbe wenye uwezo mkubwa wa kufanya vitu tofautitofauti, pia wenye uwezo wa kujibadilisha kuwa katika hali waipendayo. Asili ya imani hiyo haijajulikana vizuri, lakini ilikuwepo Uarabuni kabla ya Muhammad.

Kwa asilimia kubwa wenye imani ya uwepo wa majini wanasema ni viumbe wasioweza kuonekana, hivyo ni vigumu kupata uthibitisho wa moja kwa moja kuhusiana na viumbe hao. Kadiri ya imani hiyo majini waliumbwa na Mungu kwa kutumia moto na wakiwa wa jinsia mbili; walikuwepo tangu Adamu kuumbwa, hata enzi za Yesu majini walikuwepo, mpaka alipokuja mtume Muhamad.

Uislamu huamini kuna majini wazuri na majini wabaya kwa maana ya madhara yao katika maisha ya mwanadamu na badhi ya Waislamu (pengine wasiofuata misingi sahihi ya Uislamu) hufuga majini hao katika nyumba zao au miili yao na kuwafanya viumbe hao kama wasaidizi au walinzi wa maisha yao kwa wale ambao huamini ni majini wazuri. Lakini wengine hutumia pia majini waitwao wabaya kuharibu na kutesa maisha ya watu wengine kwa kuwatuma kuwaingia miilini na kuleta magonjwa, kuharibu kazi au biashara ya mtu na hata familia.

Hata wasio na dini na baadhi ya Wakristo hutumia majini kuponya wagonjwa na vilema na kufanya miujiza mbalimbali kama kwa mazingaombwe. Pia wapo Wakristo ambao huwatumia majini hao katika mambo yao kama vile kutafuta mali, watoto n.k.

Pamoja na hayo, Ukristo kwa jumla haupatani na imani hiyo, ila kuna madhehebu kadhaa ya Kikristo ambayo huamini uwepo wa majini kwa kuwasawazisha na mashetani. Hivyo kwao hakuna jini mzuri bali wote ni wabaya kwa kuwa wao na mashetani ni sawa, hivyo ni adui wa Mkristo yeyote yule kama alivyo Shetani mwenyewe. Wakristo wa madhehebu hayo wamekuwa wakifanya maombi kwa watu ambao wanadhaniwa kuteswa na majini ili kuwafungua kutoka katika nguvu zao za uovu, sawa na pepo ambao Bwana Yesu (mleta habari njema, yaani Injili) aliwatoa miilini mwa watu na kuwapa wanafunzi wake (wafuasi wake ambao ni Wakristo leo) mamlaka na uwezo wa kuwatoa pia.

Kwa ujumla wake, Mungu Mmoja aliye mfalme wa siku ya malipo, anaweza kukuepusha na kila jambo baya hapa duniani pasipo kuangalia wewe ni wa dini gani. Viumbe vyote ni vya Mungu na ndiye asili ya vyote, nasi tutarejea kwake.

Katika Uislamu

Kadiri ya Uislamu majini ni viumbe wa Allah kama walivyo binadamu, hivyo wanazaa, wanazaliwa na kukua, wana jinsia mbili, wapo wanamtii Mungu na waliomuasi, wana tabia kama za kwetu (uongo, dhuluma n.k.). “Na tulimuumba mtu kwa udongo unaotoa sauti unaotokana na matope yaliyotiwa sura. Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto” (Alhijra 26-27)

Kazi yao wote ni kumuabudu Mungu: “Na sikuwaumba majini na watu ila waniabudu mimi” (Adh-dhaariyaat, 51 au 56).

Tofauti ni kwamba:

  • wao wameumbwa kwa moto
  • wanasafiri haraka kuliko chombo chochote
  • wana uwezo wa kutuona wakati sisi hatuwezi kumuona ila mwenyewe akipenda kujionyesha
  • wanaweza kujibadilisha maumbile ya viumbe mbalimbali
  • wanaweza kuingia mwilini mwa mtu kwa njia ya hewa na kuathiri kiungo chochote hata kukaa katika ubongo na kumpandikiza fikra mbovu
  • wanaweza kuzini na mtu bila huyo kujitambua au kumzini bila huyo kuweza kujihami
  • wanaishi muda mrefu kuliko sisi, lakini wanaugua na kufa
  • baadhi wanajenga urafiki au uadui na watu ili wawapoteze wasipofuata sheria za Mwenyezi Mungu.

Ingawa wapo wanaoamini uwezekano wa majini kutengenezwa na watu, imani inaukanusha. “Sema: Mwenyezi Mungu ndiye muumba wa kila kitu na yeye ni mmoja mwenye kushinda” (Raad 16). Isipokuwa Waislamu wanaamini uwezekano na kuwatumia majini kwa namna mbalimbali.

Marejeo

  • Al-Ashqar, Dr. Umar Sulaiman (1998). The World of the Jinn and Devils. Boulder, CO: Al-Basheer Company for Publications and Translations.
  • Barnhart, Robert K. The Barnhart Concise Dictionary of Etymology. 1995.
  • "Genie". The Oxford English Dictionary. Second edition, 1989.
  • Abu al-Futūḥ Rāzī, Tafsīr-e rawḥ al-jenān va rūḥ al-janān IX-XVII (pub. so far), Tehran, 1988.
  • Moḥammad Ayyūb Ṭabarī, Tuḥfat al-gharā’ib, ed. J. Matīnī, Tehran, 1971.
  • A. Aarne and S. Thompson, The Types of the Folktale, 2nd rev. ed., Folklore Fellows Communications 184, Helsinki, 1973.
  • Abu’l-Moayyad Balkhī, Ajā’eb al-donyā, ed. L. P. Smynova, Moscow, 1993.
  • A. Christensen, Essai sur la Demonologie iranienne, Det. Kgl. Danske Videnskabernes Selskab, Historisk-filologiske Meddelelser, 1941.
  • R. Dozy, Supplément aux Dictionnaires arabes, 3rd ed., Leyden, 1967.
  • H. El-Shamy, Folk Traditions of the Arab World: A Guide to Motif Classification, 2 vols., Bloomington, 1995.
  • Abū Bakr Moṭahhar Jamālī Yazdī, Farrokh-nāma, ed. Ī. Afshār, Tehran, 1967.
  • Abū Jaʿfar Moḥammad Kolaynī, Ketāb al-kāfī, ed. A. Ghaffārī, 8 vols., Tehran, 1988.
  • Edward William Lane, An Arabic-English Lexicon, Beirut, 1968.
  • L. Loeffler, Islam in Practice: Religious Beliefs in a Persian Village, New York, 1988.
  • U. Marzolph, Typologie des persischen Volksmärchens, Beirut, 1984. Massé, Croyances.
  • M. Mīhandūst, Padīdahā-ye wahmī-e dīrsāl dar janūb-e Khorāsān, Honar o mordom, 1976, pp. 44–51.
  • T. Nöldeke "Arabs (Ancient)", in J. Hastings, ed., Encyclopaedia of Religion and Ethics I, Edinburgh, 1913, pp. 659–73.
  • S. Thompson, Motif-Index of Folk-Literature, rev. ed., 6 vols., Bloomington, 1955.
  • S. Thompson and W. Roberts, Types of Indic Oral Tales, Folklore Fellows Communications 180, Helsinki, 1960.
  • Solṭān-Moḥammad ibn Tāj al-Dīn Ḥasan Esterābādī, Toḥfat al-majāles, Tehran.
  • Nünlist, Tobias (2015). Dämonenglaube im Islam. Walter de Gruyter GmbH & Co KG,. ISBN 978-3-110-33168-4. 
  • Moḥammad b. Maḥmūd Ṭūsī, Ajāyeb al-makhlūqāt va gharā’eb al-mawjūdāt, ed. M. Sotūda, Tehran, 1966.

Marejeo mengine

  • Crapanzano, V. (1973) The Hamadsha: a study in Moroccan ethnopsychiatry. Berkeley, CA, University of California Press.
  • Drijvers, H. J. W. (1976) The Religion of Palmyra. Leiden, Brill.
  • El-Zein, Amira (2009) Islam, Arabs, and the intelligent world of the Jinn. Contemporary Issues in the Middle East. Syracuse, NY, Syracuse University Press. ISBN 978-0-8156-3200-9.
  • El-Zein, Amira (2006) "Jinn". In: J. F. Meri ed. Medieval Islamic civilization – an encyclopedia. New York and Abingdon, Routledge, pp. 420–421.
  • Goodman, L.E. (1978) The case of the animals versus man before the king of the Jinn: A tenth-century ecological fable of the pure brethren of Basra. Library of Classical Arabic Literature, vol. 3. Boston, Twayne.
  • Maarouf, M. (2007) Jinn eviction as a discourse of power: a multidisciplinary approach to Moroccan magical beliefs and practices. Leiden, Brill.
  • Taneja, Anand V. (2017) Jinnealogy: Time, Islam, and Ecological Thought in the Medieval Ruins of Delhi. Stanford, CA, Stanford University Press. ISBN 978-1503603936
  • Zbinden, E. (1953) Die Djinn des Islam und der altorientalische Geisterglaube. Bern, Haupt.

Viungo vya nje

Jua habari zaidi kuhusu Jini kwa kutafuta kupitia mradi wa Wikipedia Sister
Uchambuzi wa kamusi kutoka Wikamusi
Vitabu kutoka Wikitabu
Dondoo kutoka Wikidondoa
Matini za vyanzo kutoka Wikichanzo
Picha na media kutoka Commons
Habari kutoka Wikihabari
Vyanzo vya elimu kutoka Wikichuo
Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.