Jimbo katoliki la Iringa
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jimbo katoliki la Iringa (kwa Kilatini Dioecesis Iringaënsis) ni mojawapo kati ya majimbo 33 ya Kanisa Katoliki nchini Tanzania na kama hayo yote linafuata mapokeo ya Kiroma.
Makao makuu yake yako Iringa katika mkoa wa Iringa, lakini linaenea pia katika mkoa wa Mbeya.
Kanisa kuu limewekwa wakfu kwa Moyo Mtakatifu wa Yesu.
Kikanisa linahusiana na jimbo kuu la Songea kuanzia tarehe 18 Novemba 1987.
Askofu wake ni Tarcisius Ngalalekumtwa.
Parokia ni 33.
Anwani ya posta ni: P.O. Box 133, Iringa, Tanzania.
Yaliyomo |
Historia [hariri]
- 3 Machi 1922: Kuanzishwa kwa Apostolic Prefecture ya Iringa kutokana na Apostolic Vicariate ya Dar-es-Salaam
- 8 Januari 1948: Kupandishwa cheo kuwa Apostolic Vicariate ya Iringa
- 25 Machi 1953: Kufanywa dayosisi
Uongozi [hariri]
- Maaskofu wa Iringa
- Tarcisius Ngalalekumtwa (since 1992.11.21)
- Norbert Wendelin Mtega (1985.10.28 – 1992.07.06)
- Mario Epifanio Abdallah Mgulunde (1969.10.23 – 1985.03.09)
- Attilio Beltramino, I.C.M. (1953.03.25 – 1965.10.03)
- Vicar Apostolic wa Iringa
- Attilio Beltramino, I.C.M. (1948.01.08 – 1953.03.25)
- Prefect Apostolic wa Iringa
- Attilio Beltramino, I.C.M. (1936.02.18 – 1948.01.08)
- Padri Francesco Cagliero, I.C.M. (1922.05.10 – 1935)
Takwimu [hariri]
Eneo ni la kilometa mraba 43,318, ambapo kati ya wakazi 2,367,962 (2006) Wakatoliki ni 588,438 (24.9%). Mapadri ni 92, wakiwemo wanajimbo 53 na watawa 39. Kwa wastani kila mmoja anahudumia waamini 6.396. Shemasi ni 1, mabruda ni 206 na masista 549.
Viungo vya nje [hariri]
- Giga-Catholic Information
- Catholic Hierarchy
- www.catholic-hierarchy.org alla pagina [1]
- Hati Quae rei sacrae, AAS 14 (1922), uk. 221
- Hati Digna sane, AAS 40 (1948),uk. 306
- Hati Quemadmodum ad Nos, AAS 45 (1953), p. 705
- (Kiingereza) [2] kwenye www.gcatholic.com
- (Kiingereza) [3] kwenye tovuti la Baraza la maaskofu Katoliki Tanzania