Jimbo Katoliki la Sumbawanga
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jimbo Katoliki la Sumbawanga (kwa Kilatini Dioecesis Sumbavangensis) ni mojawapo kati ya majimbo 33 ya Kanisa Katoliki nchini Tanzania, na kama hayo yote linafuata mapokeo ya Kiroma.
Kanisa kuu liko mjini Sumbawanga, katika mkoa wa Rukwa.
Lilianzishwa tarehe 10 Mei 1946 na linahusiana na Jimbo Kuu la Tabora.
Askofu wa sasa ni Damian Kyaruzi.
Takwimu [hariri]
Eneo lake lote ni kama kilometa mraba 28.654, ambamo wamo wakazi 928.941. Kati yao Wakatoliki ni 607.143 (2004) yaani asilimia 65.4.
Waamini hawa wanahudumiwa na mapadri 53, ambao kati yao 49 ni wanajimbo na 4 watawa. Hivyo kwa wastani kila mmojawao anahudumia waamini 11.455.
Parokia ziko 22.
Jimbo lina mabruda 71 na masista 208.
Mlolongo wa maaskofu [hariri]
- James Holmes-Siedle, M.Afr. † (29 Julai 1946 - 5 Agosti 1958 kuhamishiwa Jimbo Katoliki la Kigoma)
- Charles Msakila † (13 Novemba 1958 - 23 Februari 1994 kufariki dunia)
- Damian Kyaruzi, tangu 21 Aprili 1997
Viungo vya nje [hariri]
- Giga-Catholic Information
- Catholic Hierarchy
- [1] katika tovuti ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania
- Bolla Quo maiora, AAS 39 (1947), uk. 80
- Bolla Quemadmodum ad Nos, AAS 45 (1953), uk. 705