Ilembula

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Kata ya Ilembula
Nchi Tanzania
Mkoa Njombe
Wilaya Wanging'ombe
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 14,451

Ilembula ni kata ya Wilaya ya Wanging'ombe katika Mkoa wa Njombe, Tanzania. Msimbo wa posta ni 59305.

Ndani ya kata kuna vijiji vya Ilembula Kati, Iponda, Igelehedza na Igula.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi wa kata walihesabiwa kuwa 14,451 [1]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 15,642 [2] walioishi humo.

Wenyeji walio wengi ni Wabena wanaolima hasa mahindi na maharagwe. Vinywaji vinavyopendwa ni ulanzi, pombe na togwa.

Ilembula Kati, Igelehedza na Igula kuna shule ya msingi.

Taasisi kubwa ni hospitali ya Kilutheri yenye vitanda 240 pamoja na chuo cha wauguzi chenye wanafunzi 143 [3].

Ilembula hukua kwa haraka kutokana na ongezeko la biashara za mazao (mahindi), viwanda vidogovidogo na kupatikana kwa huduma za kijamii kwa urahisi zaidi hasa hospitali, bidhaa muhimu za kijamii, umeme, maji na huduma za kifedha. Pia kumekuwepo ongezeko la watu katika kijiji baada ya serikali kuonyesha nia ya kukifanya kijiji cha Ilembula kuwa Mji mdogo katika wilaya hiyo ya Wanging'ombe. Hili limekuja baada ya wananchi kuomba kijiji hiko kipandishwe hadhi ili kurahisisha zaidi hupatikanaji wa huduma za kiserikali mfano TRA, mahakama na ofisi za halmashauri.

Dini[hariri | hariri chanzo]

Ilembula imekuwa kitovu cha kazi ya Walutheri katika Ubena tangu mwaka 1906, wamisionari Wajerumani walipofika. Leo hii Ilembula Kati ni makao makuu ya Jimbo la Kilutheri ndani ya Dayosisi ya Kusini KKKT.

Kanisa Katoliki lina kitovu chake kwenye kijiji cha Igelehedza pamoja na shule ya chekechea na shule ya maarifa ya nyumbani.

Madhehebu mengine, kama vile Wapentekoste, Wasabato na Mashahidi wa Yehova, wako pia hata kama si wengi.

Nao Waislamu wako: wana msikiti katika Igelehedza.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.nbs.go.tz, uk 212
  2. "Sensa ya 2012, Njombe - Wanging'ombe DC". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2004-01-02. Iliwekwa mnamo 2017-03-28. 
  3. www.ilembulanursing.ac.tz

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Kata za Wilaya ya Wanging'ombe - Tanzania

Igima | Igosi | Igwachanya | Ilembula | Imalinyi | Itulahumba | Kidugala | Kijombe | Kipengele | Luduga | Makoga | Malangali | Mdandu | Saja | Udonja | Uhambule | Uhenga | Ulembwe | Usuka | Wangama | Wanging'ombe


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Njombe bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Ilembula kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.