Kuchanyika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Hylia)
Kuchanyika
Kuchanyika wa Ulaya
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Sylvioidea (Ndege kama kucha)
Familia: Cettiidae (Ndege walio na mnasaba na kuchanyika)
Alström, Ericson, Olsson & Sundberg, 2006
Ngazi za chini

Jenasi 7:

Kuchanyika ni ndege wadogo wa familia Cettiidae. Ndege hawa wanafanana na shoro, kucha na kuchamsitu, na zamani wote waliainishwa pamoja katika familia Sylviidae. Spishi nyingine za kuchanyika zina mkia mrefu, nyingine zina mkia mfupi sana. Zina rangi ya kahawia au kijivu mgongoni na nyeupe au njano chini; spishi kadhaa zina rangi kali (Tesia k.m.). Spishi za Cettia tu zinatokea Ulaya, nyingine zinatokea misitu ya Afrika na Asia. Hula wadudu. Hulijenga tago lao kwa umbo wa kikombe au kikapu kwa kigoga, nyuzinyuzi, mizizi na/au majani. Jike huyataga mayai 2-6.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]