Hoteli za Serena
|
|
Unganisha! Imependekzwa makala hii iunganishwe na Serena Hotels. Ili kupata sababu angalia ukurasa wa majadiliano. |
| Ilipoanzishwa | 1970s in Kenya |
|---|---|
| Makao Makuu | Nairobi, |
| Bidhaa | Hotels, Lodges, and Resorts |
| Owner(s) | Tourism Promotion Services |
| Tovuti | http://www.serenahotels.com/index.asp |
Hoteli za Serena ni mnyororo wa Hotelii zinazoendeshwa nchini Afghanistan, Kenya, Msumbiji, Pakistan, Rwanda, Tanzania na Uganda. Ni mojawapo wa makampuni 96 yanayounda Aga Khan Fund for Economic Development (AKFED), sehemu ya Aga Khan Development Network (AKDN) ya kutengeneza faida. Kundi hili hufanya biashara chini ya jina Tourism Promotion Services (TPS Serena). Kampuni hii imeorodheshwa katika soko la hisa la Nairobi na ina mali 19 barani Afrika.
Yaliyomo |
Historia [hariri]
Hotelii ya Serena ya Nairobi ya Nyota tano ndio Hotelii kuu zaidi katika kundi la Hotelii za Serena. Inashirikisha vyumba 183 na vyumba vikuu (“Suites”) 7, pamoja na jumba kuu moja la Rais. Klabu ya Maisha Health, kwa ubishano, ndio bora zaidi nchini Afghanistan. Pamoja na mali zingine kadhaa za Serena, Hotelii hii ni mwanachama wa Hotelii zinaongoza Duniani.
Hoteli ya Nyota tano ya Serena katika mji mkuu wa Islamabad nchini Pakistan ilichorwa na mbunifu maarufu kutoka Pakistani, Nayyar Ali Dada na ilifunguliwa mwaka wa 2002. Inashirikisha vyumba 220 pamoja na vyombo vilivyotengenezwa kwa hali ya usanaa, "ballroom"(sehemu rasmi iliyotengwa kwa ajili ya kucheza kwa sababu ya muziki unaovutia) ya watu 200, mikahawa tatu ya kipekee, duka la kununua bidhaa na klabu ya afya lenye sehemu ya kuogelea. Sakafu ya juu ya hoteli hii inasehemu ya karamu na sehemu kubwa la nyasi lenye uwezo wa kushikilia wageni 1000. Pia ni mwanachama wa Hoteli zinazoongoza Duniani.
Hoteli ya Serena ya Kampala ni hoteli ya nyota tano iliyozungukwa na [1] ya mabustani na eneo kubwa lenye nyasi nzuri zilizosawa. Hoteli hii ina helipad (sehemu ambayo ndege aina ya helikopta hutua) ya kibinafsi. Hoteli hii pia inajivunia makao 152 ya kibinafsi, pamoja na vyumba 32 ya utendaji na vyumba kuu (Suites) 12, moja ambayo ni ya rais. Hoteli hii ilikuwa sehemu ambao ilichaguliwa kuwa mwenyeji wa Malkia Elizabeth wa II wakati wa mkutano wa Wakuu wa serikali ya Jumuiya ya Madola mwaka wa 2007 (CHOGM 2007). Karibu na Hotelii hii ni kituo cha mkutano cha kimataifa cha Serena cha Kampala ambacho kina uwezo cha kushikilia wajumbe 1500 na uwezo wa kutafsiri kisamtidiga hadi lugha tisa.
Mapema mwaka wa 2007, Serena ilichukua usimamizi wa mali mbili nchini Rwanda kutoka Southern Sun. Hoteli Hizi zimebadilishwa majina kuwa Hoteli ya Serena ya Kigali na Hoteli ya Serena ya Ziwa Kivu.
Hoteli ya Nyota tano ya Serena ya Kabul ilifunguliwa katika mji mkuu wa Kabul, Afghanistan mwaka wa 2005, na zingine kwa sasa zinapangiwa kufunguliwa katika miji mikuu ya Afghanistan ya Mazar-e-Sharif na Herat. Mnamo 14 Januari 2008, Hoteli ya Serena ya Kabul nchini Afghanistan ilikuwa shabaha ya mashambulizi ya ugaidi na ilijumuisha wauaji wanaotumia bomu, magaidi wanaotumia bunduki aina ya “machine-gun” na magaidi wenye bomu ya aina ya “grenade”. Watu saba waliuawa katika shambulio hilo, wakiwa ni pamoja na mwandishi wa habari kutoka Norwayna raia wa Marekani. . Taliban mmoja alidai wajibu.
Mali ya Serena barani Afrika [hariri]
- Kenya
- Mombasa
- Nairobi(Mji Mkuu)
- Mlima Kenya
- Masai Mara
- Amboseli
- Samburu
- Nanyuki
- Uganda
- Kampala
- Ziwa Victoria, Lweeza
Mali ya Serena barani Asia [hariri]
- Afghanistan
- Kabul
- Herat (yaja hivi karibuni)
- Mazari Sharif (yaja hivi karibuni)
- Tajikistan
- Dushanbe (yaja hivi karibuni)
Viungo vya nje [hariri]
Angalia Pia [hariri]
- Aga Khan Fund for Economic Development
- Aga Khan Development Network
- Soko la Hisa la Nairobi
Marejeo [hariri]
| Makala African corporation or company bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |
| Makala hii kuhusu maeneo ya Kenya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Hoteli za Serena kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |