Homa ya matumbo
Homa ya matumbo husababishwa na bakteria anayeitwa Salmonella Typhi. Ugonjwa huu huambukizwa kwa mtu kula au kunywa chakula au maji yalio na kinyesi cha mu aliyambukizwa.[1] Bakteria hawa hutoboa na kunyonya chakula kwenye matumbo ya binadamu.
Yaliyomo |
[hariri] Dalili
- Homa kali
- Kutoka kwa majasho mengi
- Kuharisha (bila ya kutoa damu)
- Mara nyingine, vitone vyekundu huonekana kwenye mwili.
Kwa kawaida, homa ya matumbo isipotibiwa hugawanyika katika hatua nne, kila hatua ikichukua takriban wiki moja.
Katika wiki ya kwanza:
- Joto la mwili huongezeka
- Kichwa huuma
- Kukohoa
- Damu kutoka kwa pua, ingawa tukio hili huwa ni nadra kutokea.
- Maumivu ya tumbo pia huweza kutokea
Katika wiki ya pili:
- Homa huongezeka
- Mgonjwa huanza kupagawa, kama mwenda wazimu
- Vitone vyekundu huanza kutokea kwenye kifua
- Mgonjwa huharisha, takriban mara sita au nane kwa siku.
- Kutapika kwa mgonjwa
- Ini la mgonjwa huvimba
- Homa ya mgonjwa huongezeka katika wakati wa alasiri kwenye wiki ya kwanza na ya pili.
Wiki ya tatu:
- Matumbo hutoa damu.
- Matumbo hutoboka
Wiki ya tatu ikimalizika, homa huanza`kutilia. Hii huendelea hadi wiki ya nne.
[hariri] Matibabu
Mara nyingi, homa ya matumbo haiuwi binadamu. Dawa kama ampicillin, chloramphenicol, trimethoprim-sulfamethoxazole, Amoxicillin and ciprofloxacin hutumika kutibu wagonjwa katika nchi zilizoendelea.
[hariri] Hatua za kuzuia kupata homa hii
- Usafi wa mazingara na wa kibinafsi ni hatua bora ya kujikina kutokamana na ugonjwa huu.
- Homa ya matumbo haiathiri wanyama kwa hivyo maambukizi ni kutoka kwa binadamu mmoja hadi mwingine.
- Homa hii hueza kuenea kwenye mazingara ambayo kinyesi cha binadamu hutangamana na vyakula vyao. Upishi wa makini na uoshaji mikono ni kingo bora zaidi kwa kuzuia maradhi haya kuenea.
- Chanjo ni za aina mbili: moja inayotiwa kwa njia ya mdomo iitwayo Ty21a (au Vivotif Berna) na nyingine ya sindano kwa majina Typhim Vi iliyotengenezwa na Sanofi Pasteur au Typherix iliyotengenezwa na GlaxoSmithKline.
[hariri] Historia
Mnamo mwaka 2004-05, janga la homa ya matumbo lilizuka katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo iliyoathiri watu 42,000 na kuuwa watu 214 (kulingana na ripoti ya shirika la World Health Organisation).
[hariri] Waathiriwa maarufu
- Mary Mallon, aliyejulikana kama Typhoid Mary.
- Louisa May Alcott, mwandishi wa Little Women.
- Charles Darwin, mwanasayansi, aliathirika pindi alipoenda nchini Chile mnamo 1835.
- Eugenia Tadolini, alikufa mjini Paris mnamo 1872.
- William Wallace Lincoln, mtoto wa tatu wa Abraham Lincoln, ambaye ni rais wa 16 wa Marekani, pamoja na Mary Todd Lincoln, walifariki kutokana na maradhi haya mnamo February 20, 1862.
- Wilbur Wright, alikufa mnamo May 30, 1912 baada ya kuugua homa hii.
[hariri] Marejeo
- ↑ Giannella RA (1996). "Salmonella", Baron's Medical Microbiology (Baron S et al., eds.), 4th, Univ of Texas Medical Branch. ISBN 0-9631172-1-1.
[hariri] Kusoma zaidi
- Easmon C (2005-04-01). Typhoid fever and paratyphoid fever. Travel Health. Rudishwa juu ya 2008-10-05.
- Harrison NG. Walter Reed and Typhoid Fever, 1897–1911. Univ of Virgina. Retrieved on 2008-10-05.
- Nicolson publisher=BBC News, Stuart. "Typhoid left city (Aberdeen) 'under siege'", 2008-06-26. Retrieved on 2008-10-05.
- O'Hara C. "Typhoid Fever Led To The Fall Of Athens", Elsevier, 2006-01-26. Retrieved on 2008-10-05.

