Historia ya Kenya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Historia ya Kenya inahusu eneo la Afrika Mashariki ambalo wakazi wake leo wanaunda Jamhuri ya Kenya.

Historia ya Kenya kama nchi inayokaliwa na binadamu, inaenea miaka laki kama si milioni kadhaa. Kumbe historia yake kama nchi huru ni fupi.

Historia ya awali[hariri | hariri chanzo]

Uvumbuzi wa majuzi karibu na Ziwa Turkana unaonyesha kwamba kiumbe kama Australopithecus anamensis aliishi katika eneo ambalo sasa ni Kenya kuanzia miaka milioni 4.1 iliyopita.

Lakini mabaki yaliyopatikana katika mabonde ya Tugen, yaliyokuwa na takriban miaka milioni 6, yalipelekea kutajwa kwa aina mpya ya spishi, Orrorin tugenensis.

Ustaarabu wa mapema Kenya[hariri | hariri chanzo]

Mahali pa Msikiti Mkuu wa Gedi, karne ya 13.

Wakazi wa kwanza wa eneo linaloitwa Kenya walikuwa wa jamii ya Wakhoisan: hadi leo kuna makabila matatu madogo yenye asili hiyo, ingawa yanatumia lugha za Kikushi: Waata, Waawer na Wadahalo.

Wakushi kutoka kaskazini waliingia Kenya miaka ya 2000 KK.[1] Wakushi kutoka Afrika kaskazini waliingia eneo linaloitwa Kenya miaka ya 2000 KK.[1]

Katika milenia ya 1, wazungumzaji wa lugha za Kinilo-Sahara na lugha za Kibantu waliingia katika eneo hili, na sasa Waniloti ni 30% ya Wakenya wote. Pwani ya Kenya ikawa makao ya jamii ya wahunzi na jamii ya wakulima wadogo wadogo, wawindaji na wavuvi ambao walikuwa mhimili wa uchumi kwa kushirika katika kulimo, uvuvi, utengenezaji chuma, na kufanya biashara na nchi za kigeni.[1]

Kuanzia karne ya 6 au karne ya 9, Kenya ilijihusisha na shughuli za ubaharia kukuza uchumi ikaanza kutengeneza meli za kuabiria kusini hadi miji mingine yenye bandari kama Kilwa na Shanga iliyo katika pwani ya Afrika Mashariki.

Wafanyabiashara Waarabu walianza kwenda pwani ya Kenya mara kwa mara karne ya 1 BK. Kenya ilikuwa karibu na Peninsula ya Arabia na hii ilialika ukoloni.

Makazi ya Waarabu na Waajemi yaliongezeka kandokando ya pwani kufikia karne ya 8. Hata hivyo, baadhi ya walioitwa "Waarabu" katika eneo la Afrika Mashariki walikuwa machotara, Waafrika-Waarabu.

Kuanzia karne ya 6 au karne ya 9, Kenya ilijihusisha na shughuli za ubaharia kukuza uchumi ikaanza kutengeneza meli za kuabiria kusini hadi miji mingine yenye bandari kama Kilwa na Shanga iliyo katika pwani ya Afrika Mashariki.

Mombasa ulikuwa mji wenye bandari wa nchi ya Kenya kabla ya ukoloni katika Enzi ya kati. Bandari hiyo ilitumika kuendeleza biashara na miji mingine yenye bandari Afrika, Uajemi, na wafanyabiashara Waarabu, Yemeni na hata Bara Hindi.[2]

Baharia Mreno Duarte Barbosa wa karne ya 15 alidai kuwa "[Mombasa] ni bandari nzuri na yenye shughuli nyingi, mashua nyingi na hata meli kubwa ajabu, ambazo zote hutoka Sofala na nyingine kutoka Cambay, Melinde na nyingine zinazoabiri hadi kisiwani Unguja."[3]

Kiswahili, ambayo ni lugha ya Kibantu iliyokopa misamiati ya Kiarabu, Kiajemi na mingine kutoka Mashariki ya Kati na Asia Kusini, baadaye ilikua ikawa lingua franca ya kibiashara kwa jamii mbalimbali.[1]

Kwa karne nyingi, upwa wa Kenya umekuwa mwenyeji wa wafanyabiashara na wasafiri. Kati ya miji iliyopo kwenye upwa wa Kenya ni mji wa Malindi. Umebakia kuwa makazi muhimu ya Waswahili tangu karne ya 14 na wakati mmoja ulishindana na Mombasa kwa ukuu pande hizi za Afrika Mashariki. Kwa kawaida, Malindi umekuwa mji na bandari ya kirafiki kwa serikali zingine.

Mwaka wa 1414, Sultani Mwarabu wa Malindi alianzisha uhusiano wa kidiplomasia na utawala wa Uchina wa Ming, wakati wa safari za mchunguzi Zheng He.[4] Katika mwaka wa 1498, utawala wa Malindi ulimkaribisha msafiri na mvumbuzi maarufu kutoka Ureno, Vasco da Gama.

Karne kadhaa kabla ya ukoloni, upwa wa Kenya wanakoishi Waswahili ulikuwa sehemu ya eneo la mashariki mwa Afrika lililofanya biashara, hasa ya watumwa na pembe za ndovu na Waarabu na Wahindi. Inasemekana kwamba kabila la Wameru lilitokana na watumwa waliotoroka utumwa Uarabuni miaka ya 1700. Mwanzoni wafanyabiashara wengi walitoka milki za Uarabuni lakini baadaye wengine wakatoka Unguja (kama Tippu Tip).[5]

Ujio wa Wazungu[hariri | hariri chanzo]

Utamalaki wa Waarabu katika eneo la pwani ulipitwa karne ya 16 na Wareno ambao utawala wao pia ulipisha ule wa Omani mwaka wa 1698.

Kabla ya hapo mwaka 1652 Mholanzi, kwa jina Jan van Riebeeck, alianzisha mji wa Cape Town kwa niaba ya Kampuni ya Kiholanzi inayopatikana Mashariki ya Nchi ya India. Kampuni hii ilihitaji kituo kwa ajili ya jahazi zake zilizosafiri kati ya Ulaya na visiwa vya Indonesia.

Baada ya miaka kadhaa Waingereza walinyakua eneo hili rasmi mwaka wa 1806. Hali hii ilitambuliwa na Uholanzi mwaka 1815 kwenye Mkutano wa Vienna. Koloni la Rasi liliendelea chini ya Uingereza hadi mwaka 1910.

Uingereza ulieneza zaidi mvuto wake karne ya 19 kupitia wamisionari. Misheni ya kwanza ya Ukristo ilianzishwa tarehe 25 Agosti mwaka wa 1846, na Daktari Ludwig Krapf, Mjerumani na mtawa wa Church Missionary Society ya Uingereza, ambaye alijifahamisha kati ya Wamijikenda huko pwani. Baadaye alitafsiri Biblia kutoka Kiingereza hadi Kiswahili.

Historia ya ukoloni[hariri | hariri chanzo]

Historia ya ukoloni ya Kenya ilianza wakati milki ya Ujerumani ya nchi lindwa (protectorate) ilipoanzishwa. Nchi lindwa hii ilikuwa mali ya Sultani wa Pwani na Zanzibar na wakati huo ulikuwa mnamo 1885.

Hii ilifuatiwa na kuwasili kwa British East Africa Company (BEAC) ya William Mackinnon mwaka wa 1888, baada ya kampuni hiyo kupokea mkataba wa kifalme na haki za kuungama kwa pwani ya Kenya kutoka Sultani wa Zanzibar kwa kipindi cha miaka 50.

Uhasimu wa umilki ulianza kuonekana wakati Ujerumani ulipatiana sehemu yake ya pwani kwa milki ya Uingereza mwaka wa 1890, ili uweze kuidhibiti pwani ya Tanganyika.

Kuhozi kwa ukoloni huu mara kwa mara ulikumbana na upinzani mbalimbali: Waiyaki wa Hinga, chifu Mkikuyu aliyetawala Dagoretti, ambaye alikuwa amesaini mkataba na Frederick Lugard wa BEAC, baada ya kuteswa na kubughudhiwa, aliliteketeza gereza la Lugard mnamo 1890. Waiyaki miaka miwili baadaye alitekwa nyara na kuuawa na Waingereza.

Kufuatia matatizo ya kifedha ya British East African Company, serikali ya Uingereza ilianzisha utawala wa moja kwa moja kupitia nchi lindwa ya Afrika ya mashariki (East African Protectorate) tarehe 1 Julai 1895.

Hii ilifuatwa na ufunguzi wa nyanda kwa Wazungu walowezi mwaka wa 1902. Ujenzi wa reli ulianza mwaka wa 1895 kutoka Mombasa hadi Kisumu katika ziwa Viktoria na ulimalizika mwaka wa 1901. Ujenzi huo uliwezesha wakoloni hao kuingia ndani kabisa mwa Kenya. Hii ilikuwa sehemu ya kwanza ya reli ya Uganda.

Katika ujenzi wa reli, Waingereza walikumbana na upinzani mgumu, hasa kutoka kwa Koitalel Arap Samoei, kiongozi wa Kinandi na mwaguzi aliyetabiri ya kwamba nyoka mweusi atapita katikati ya eneo la Nandi akitema mate ya moto. Nyoka alikuwa anaashiria reli. Kwa miaka kumi Samoei alipigana dhidi ya wajenzi wa reli na gari la moshi. Baadaye, Samoei aliuawa na Waingereza kwani walikuwa na dhamira ya kuendelea na kumaliza reli hii.

Walowezi waliruhusiwa kuingia bungeni na serikali mwaka wa 1907 kupitia Legislative Council, shirika la Ulaya ambalo baadhi ya walowezi waliasisiwa na wengine walichaguliwa. Lakini tangu mamlaka zaidi zilibakia katika mikono ya Gavana, walowezi walitaka Kenya ibadilishwe kuwa koloni la kiarauni au taji (Crown Colony), ambayo ilimaanisha mamlaka zaidi kwa walowezi.

Walowezi hao walihitimu lengo lao mwaka wa 1920 kwa kulifanya Baraza liwakilishwe na walowezi zaidi. Waafrika walitengwa kutoshiriki katika siasa ya moja kwa moja hadi mwaka wa 1944, ambapo mmojawao aliingizwa kwenye Baraza.

Wakikuyu waliamua kuanzisha chama chao cha kwanza cha harakati za kisiasa ambacho kiliitwa Young Kikuyu Association. Kiongozi wake alikuwa Harry Thuku. Sababu nyingine ya kuanzishwa kwa chama hiki ni kwamba Waafrika hawakuwa na mwakilishi katika siasa. Chama hicho kilianzishwa mwaka wa 1921. Baadaye jina la chama lilibadilishwa likawa Kenya African Union (KAU), shirika la kitaifa lilodai kuingia katika nchi iliyomilikwa na walowezi. Mwaka 1947, urais wa chama hiki ulitolewa kwa Jomo Kenyatta.

Kuanzia Oktoba 1952 mpaka Desemba 1959, Kenya ilikuwa katika hali ya hatari kufuatia uasi wa Mau Mau dhidi ya utawala wa Uingereza. Ushiriki wa Afrika katika mchakato wa kisiasa uliendelea kwa kasi katika sehemu ya mwisho ya muda huo kwani Waingereza walitaka kutenga wahalifu na wafuasi wao. Uchaguzi wa kwanza wa moja kwa moja wa Waafrika katika bunge ulifanywa mwaka wa 1957.

Kenya huru[hariri | hariri chanzo]

Licha ya Waingereza kuwa na matumaini ya kuwapa wapinzani Waafrika mamlaka "ya wastani" zaidi, ilikuwa Kenya African National Union (KANU) ya Jomo Kenyatta, mwanachama wa kabila la Kikuyu na mfungwa wa zamani, ambayo iliunda serikali muda mfupi kabla ya Kenya kupata uhuru tarehe 12 Desemba 1963.

Mwaka mmoja baadaye, Kenya ikawa jamhuri na Waziri mkuu Mzee Jomo Kenyatta akawa Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Kenya.

Chama kidogo cha Kenya African Democratic Union (KADU), kilichowakilisha muungano wa makabila madogo ambayo yaliogopa utawala wa makabila makubwa, kilijitoa na kujivunja mwaka wa 1964 na wanachama wake wakajiunga na KANU.

Chama kidogo cha upinzani, Kenya People's Union (KPU), kilianzishwa mwaka 1966, kiongozi wake akiwa Jaramogi Oginga Odinga aliyewahi kuwa makamu wa rais Kenyatta. KPU ilipigwa marufuku, na kiongozi kuwekwa kizuizini baada ya chachari za kisiasa zilizohusishwa na ziara za Kenyatta katika Mkoa wa Nyanza. Hakuna vyama vingine vya upinzani vilivyoanzishwa baada ya 1969, kupelekea Kenya kuwa mfumo wa chama kimoja chini ya KANU.

Wakati wa kifo ya Kenyatta (22 Agosti 1978), Makamu wa Rais Daniel Arap Moi, akawa rais wa mpito. Tarehe 14 Oktoba, Moi akawa rais rasmi baada ya kuchaguliwa kama mkuu wa KANU na mteule wake pekee.

Mwezi Juni mwaka wa 1982, bunge lilirekebisha katiba na kufanya rasmi Kenya kuwa nchi ya chama kimoja.

Tarehe 1 Agosti wanachama wa Kenya Air Force walizindua jaribio la mapinduzi, ambalo lilisimamishwa mara moja na vikosi vilivyoongozwa na Jeshi, General Service Unit (GSU) - sehemu ya polisi - na baadaye polisi wa kawaida, lakini si bila ya majeruhi.

Siasa ya vyama vingi[hariri | hariri chanzo]

Baada ya shinikizo kutoka ndani na nje ya nchi, bunge lilifutilia mbali sehemu ya katiba kuhusu chama kimoja mnamo Desemba 1991.

Uchaguzi wa vyama vingi vya kisiasa wa Desemba 1992 ulimpa Rais ushindi chini ya chama cha KANU kwa kupata viti vingi. Rais Moi alichaguliwa tena kwa muda wa miaka mitano, ingawa vyama vya upinzani vilishinda asilimia 45 ya viti vya bunge. Harakati ya demokrasia ya Kenya ilivunjika kabla ya uchaguzi, hivyo basi kuisaidia KANU kubaki madarakani.

Afu zaidi mnamo Novemba 1997 uliruhusu upanuzi wa vyama vya kisiasa kuanzia 11 hadi 26. Rais Moi alishinda upya kama Rais katika uchaguzi wa Desemba 1997, na chama chake cha KANU kilihifadhi viti vingi vya bunge.

Kenya, miaka ya hivi majuzi[hariri | hariri chanzo]

Uchaguzi wa mwaka 2002[hariri | hariri chanzo]

Kwa kuzuiwa kikatiba kugombea katika uchaguzi wa urais wa Desemba 2002, Moi alimpendekeza Uhuru Kenyatta, mtoto wa Rais wa kwanza wa Kenya, kama mrithi wake. Muungano wa Rainbow Coalition wa vyama vya upinzani ulikishinda chama tawala cha KANU, na kiongozi wake, makamu wa rais wa zamani wa Moi Mwai Kibaki, alichaguliwa kuwa rais kwa kura nyingi.

Mnamo tarehe 27 Desemba 2002, kwa asilimia 62 wapiga kura walichagua kwa wingi wanachama wa Muungano wa NaRC bungeni na mgombea wa NaRC Mwai Kibaki kuwa rais. Wapiga kura walimkataa mgombea urais wa Kenya African National Union (KANU), Uhuru Kenyatta, mgombea mteule wa rais anayeondoka Moi. Waangalizi wa kimataifa na wa ndani waliripoti uchaguzi wa 2002 kuwa wa haki zaidi na usio na vurugu zaidi kuliko ule wa 1992 na 1997. Kuonyesha kwake nguvu kulimruhusu Kibaki kuchagua baraza la mawaziri, kutafuta uungwaji mkono wa kimataifa na kusawazisha mamlaka ndani ya NaRC.

Mitindo ya kiuchumi[hariri | hariri chanzo]

Kenya ilishuhudia kuimarika kwa uchumi kwa kuvutia, kusaidiwa na mazingira mazuri ya kimataifa. Kiwango cha ukuaji wa kila mwaka kiliimarika kutoka -1.6% mwaka 2002 hadi 2.6% ifikapo 2004, 3.4% mwaka 2005, na 5.5% mwaka 2007. Hata hivyo, tofauti za kijamii pia ziliongezeka; manufaa ya kiuchumi yalikwenda kinyume na wale waliokuwa tayari wenye uwezo (hasa Wakikuyu); ufisadi ulifikia kina kipya, ukilingana na udhalilishaji wa miaka ya Moi. Hali ya kijamii ilizorota kwa Wakenya wa kawaida, ambao walikabiliwa na wimbi kubwa la uhalifu wa kawaida katika maeneo ya mijini; vilianzisha vita kati ya makabila yanayopigania ardhi; na ugomvi kati ya polisi na dhehebu la Mungiki, ambao ulisababisha vifo vya zaidi ya watu 120 mnamo Mei-Novemba 2007 pekee.

Uchaguzi wa 2007 na vurugu za kikabila[hariri | hariri chanzo]

Mara baada ya kuonekana kama "wenye matumaini makubwa zaidi duniani," utawala wa Kibaki ulipoteza nguvu zake haraka kwa sababu ulihusishwa kwa karibu sana na vikosi vya Moi vilivyokataliwa. Mwendelezo kati ya Kibaki na Moi uliweka mazingira ya kujiangamiza kwa Muungano wa Kitaifa wa Upinde wa mvua wa Kibaki, ambao ulitawaliwa na Wakikuyu. Vikundi vya Magharibi vya Luo na Kalenjin, vinavyodai uhuru zaidi, vilimuunga mkono Raila Amolo Odinga (1945-) na Orange Democratic Movement (ODM) yake.

Katika uchaguzi wa Desemba 2007, Odinga, mgombea wa ODM, alishambulia kushindwa kwa utawala wa Kibaki. ODM iliwashtaki Wakikuyu kwa kunyakua kila kitu na makabila mengine yote kupoteza; kwamba Kibaki alikuwa amesaliti ahadi zake za mabadiliko; kwamba uhalifu na vurugu havikudhibitiwa, na kwamba ukuaji wa uchumi hauleti manufaa yoyote kwa mwananchi wa kawaida. Katika uchaguzi wa Desemba 2007 ODM ilishinda viti vingi katika Bunge, lakini kura za urais zilikumbwa na madai ya kuibiwa kwa pande zote mbili. Huenda isijulikane kamwe ni nani aliyeshinda uchaguzi, lakini ilikuwa takriban 50:50 kabla ya wizi kuanza.

"Majimboism" ilikuwa ni falsafa iliyoibuka katika miaka ya 1950, ikiwa na maana ya shirikisho au kanda kwa Kiswahili, na ilikusudiwa kulinda haki za wenyeji, hasa kuhusu umiliki wa ardhi. Leo "majimboism" ni kanuni kwa baadhi ya maeneo ya nchi kutengwa kwa ajili ya makabila maalum, kuchochea aina ya mauaji ya kikabila ambayo yameenea nchi tangu uchaguzi. Majimbo daima imekuwa na wafuasi wengi katika Bonde la Ufa, kitovu cha ghasia za hivi majuzi, ambapo wenyeji wengi kwa muda mrefu wamekuwa wakiamini kwamba ardhi yao iliibiwa na watu wa nje. Uchaguzi wa Desemba 2007 ulikuwa kwa sehemu ya kura ya maoni kuhusu majimboism. Iliwakutanisha wanamajimbo wa leo, akiwakilishwa na Odinga, ambaye alipigania ukandamizaji, dhidi ya Kibaki, ambaye alisimama kwa hali ya sasa ya serikali kuu ambayo imeleta ukuaji mkubwa wa uchumi lakini mara kwa mara imeonyesha matatizo ya nguvu nyingi iliyojilimbikizia mikononi mwa wachache - rushwa, upweke, upendeleo na upande wake mbaya, kubaguliwa. Katika mji wa Londiani katika Bonde la Ufa, wafanyabiashara wa Kikuyu waliishi miongo kadhaa iliyopita. Mnamo Februari 2008, mamia ya wavamizi wa Kalenjin walimiminika kutoka kwenye vilima vilivyo karibu na kuchoma shule ya Kikuyu. Wanachama laki tatu wa jamii ya Wakikuyu walifukuzwa kutoka jimbo la Bonde la Ufa. Wakikuyu walilipiza kisasi haraka, wakajipanga katika magenge yaliyojihami kwa vyuma na miguu ya mezani na kuwawinda Wajaluo na Wakalenjin katika maeneo yenye Wakikuyu kama Nakuru. "Tunafikia toleo letu potovu la majimboism," aliandika mmoja wa waandishi mashuhuri wa Kenya, Macharia Gaitho.

Wajaluo wa kusini-magharibi walikuwa wamefurahia nafasi nzuri wakati wa ukoloni wa marehemu na kipindi cha uhuru wa mapema wa miaka ya 1950, 1960 na mapema miaka ya 1970, hasa katika suala la umaarufu wa wasomi wake wa kisasa ikilinganishwa na wale wa makundi mengine. Hata hivyo Wajaluo walipoteza umaarufu kutokana na mafanikio ya Wakikuyu na makundi yanayohusiana nao (Embu na Meru) katika kupata na kutumia mamlaka ya kisiasa wakati wa enzi ya Jomo Kenyatta (1963–1978). Ingawa vipimo vya umaskini na afya mwanzoni mwa miaka ya 2000 vilionyesha Wajaluo wasiojiweza ikilinganishwa na Wakenya wengine, kuongezeka kwa uwepo wa wasio Wajaluo katika taaluma hiyo kulionyesha kudhoofika kwa wataalamu wa Waluo kutokana na kuwasili kwa wengine badala ya kupungua kabisa kwa idadi ya Wajaluo.

Urais wa Uhuru Kenyatta (2013-2022)[hariri | hariri chanzo]

Rais wa 3 wa Kenya Mwai Kibaki alitawala tangu 2002 hadi 2013. Baada ya uongozi wake Kenya ilifanya uchaguzi wake mkuu wa kwanza baada ya katiba mpya kupitishwa mwaka wa 2010. Uhuru Kenyatta (mtoto wa rais wa kwanza Jomo Kenyatta) alishinda katika matokeo ya uchaguzi yaliyobishaniwa, na kusababisha maombi ya kiongozi wa upinzani, Raila Odinga. Mahakama ya juu zaidi iliidhinisha matokeo ya uchaguzi na Rais Kenyatta alianza muhula wake na William Ruto kama naibu rais. Licha ya matokeo ya uamuzi huu, Mahakama ya Juu na mkuu wa Mahakama ya Juu walionekana kuwa taasisi zenye nguvu ambazo zingeweza kutekeleza jukumu lao la kukagua mamlaka ya rais. Mnamo 2017, Uhuru Kenyatta alishinda muhula wa pili afisini katika uchaguzi mwingine uliokumbwa na utata. Kufuatia kushindwa huko, Raila Odinga aliomba tena matokeo katika Mahakama ya Juu, akiituhumu tume ya uchaguzi kwa usimamizi mbaya wa uchaguzi na Uhuru Kenyatta na chama chake kwa udanganyifu. Mahakama ya Juu ilibatilisha matokeo ya uchaguzi katika uamuzi uliokuja kuwa wa kihistoria barani Afrika na mojawapo ya maamuzi machache sana duniani ambayo matokeo ya uchaguzi wa urais yalibatilishwa. Uamuzi huu uliimarisha nafasi ya Mahakama ya Juu kama chombo huru. Kwa hivyo, Kenya ilikuwa na duru ya pili ya uchaguzi wa nafasi ya urais, ambapo Uhuru aliibuka mshindi baada ya Raila kukataa kushiriki, akitaja kasoro.

Kusalimiana kwa mikono mnamo Machi 2018 kati ya rais Uhuru Kenyatta na mpinzani wake wa muda mrefu Raila Odinga kulimaanisha upatanisho uliofuatwa na ukuaji wa uchumi na kuongezeka kwa uthabiti.

Urais wa William Ruto (2022-)[hariri | hariri chanzo]

Mnamo Agosti 2022, Naibu Rais William Ruto alishinda uchaguzi wa urais. Alichukua 50.5% ya kura. Mpinzani wake mkuu, Raila Odinga, alipata 48.8% ya kura. Kulingana na utafiti wa Afrobarometer 67.9% ya raia wa Kenya walishiriki katika uchaguzi uliopita(2022) na 17.6% hawakupiga kura katika uchaguzi wa urais. Mnamo tarehe 13 Septemba 2022, William Ruto aliapishwa kama rais wa tano wa Kenya.

Angalia pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Historia ya Kenya kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.