Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Magharibi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Faili:Tsavo West National Park, lake.jpg
Ziwa katika Hifadhi ya Kitaifa ya Tsavo Magharibi
Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Magharibi
Mahali pa Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Magharibi
MahaliKenya
Coordinates

3°19′30″S 38°8′29″E / 3.32500°S 38.14139°E / -3.32500; 38.14139Coordinates: 3°19′30″S 38°8′29″E / 3.32500°S 38.14139°E / -3.32500; 38.14139{{#coordinates:}}: cannot have more than one primary tag per page

Eneo9,065 km²
Kuanzishwa1948
Mamlaka ya utawalaKenya Wildlife Service

Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Magharibi (Tsavo West National Park) iko katika Mkoa wa Pwani ya Kenya. Mbuga hii ina upana wa eneo a eneo wa kilomita 9,065. Barabara ya A109 barabara ya Nairobi - Mombasa na reli hugawanya mbuga katika sehemu mbili za mashariki na magharibi. Sehemu ya magharibi ni maarufu zaidi kutokana na mandari yake yanayovutia zaidi kama vile Chemichemi ya Mzima, wanyamapori mbalimbali, mfumo mzuri wa barabara, hifadhi ya vifaru, uwezo wa kupanda mwamba na wageni huongozwa wakati wanatembea kando ya mto Tsavo. Mbuga hii inaendeshwa na Shirika la Huduma kwa Wanyama Pori la Kenya(maarufu kama Kenya Wildlife Service).

Akiolojia / Historia[hariri | hariri chanzo]

Ingawa maeneo chache za akiolojia za enzi za Stone Age na Middle Stone Age zimeandikwa kutoka ardhi inayopatikana katika Tsavo, kuna ushahidi zaidi uchumi uliyoendelea wa Late Stone Age kutoka miaka 6,000 hadi 1,300 iliyopita. Utafiti umeonyesha kwamba maeneo ya akiolojia kuhusu maisha ya kale hupatikana karibu na Mto Galana kwa wingi. Wenyeji wa maeneo haya waliwinda wanyama pori, walivua samaki na pia kufunga wanyama wa kinyumbani. Kwa sababu ya upungufu wa maji kutoka mto Galana, makazi ya binadamu katika Tsavo yalilenga maeneo yanayomiliki bonde hilo na katika eneo wazi ukielekea upande wa magharibi.

Wafanyabiashara waswahili walifanya biashara na wenyeji wa Tsavo kwa kuhuza na kununua pembe za ndovu,ngozi za wanyamapori, na pengine watumwa mnamo miaka 700 baada ya kifo cha kristo (na pengine mapema). Hakuna ushahidi wa moja kwa moja ya kuonyesha kwamba waswahili walikuwa wakoloni wa eneo la Tsavo. Badala yake, biashara iliimarishwa kwa kupelekwa kwa bidhaa kwenda na kutoka Pwani ya Swahili kupitia mtandao wa jamii. Biashara ya bidhaa kama vile gamba za kaa na mbanyoa zimepatikana katika maeneo ya akiolojia na zinasemekana kuwa zimekuwa tangu mapema kipindi cha uswahili.

Karne ya kumi na tisa, Wapelelezi kutoka Uingereza na Ujerumani walirekodi kuwa watu ambao sasa tunawaita Orma na Waata wakati wa safari zao kupitia "nyika," walionekana kama maadui katika maslahi yao. Kuanzia mwisho wa karne ya kumi na tisa / na mapema karne ya ishirini, Waingereza walianza juhudi za pamoja kuwa wakoloni wa ndani ya Kenya na wakajenga reli ya Uganda kupitia Tsavo mwaka wa 1898. Ujenzi ulikwama kwa muda kwa sababu "simba walao wandamu" waliwashambulia wajenzi wa reli na simba hao walijulikana baada kama wala watu wa Tsavo.

Tsavo ilibakia ya nchi kwa wafugaji wa Orma na Wamasai na wawindaji na wakusanyaji wa Waata hadi mwaka wa 1948, wakati ilikubaliwa rasmi kama Mbuga ya Kitaifa. Wakati huo, idadi ya wazawa ilihamishwa kwa maeneo ya Mtito Andei na Voi na vilevile maeneo mengine karibu na Vilima vya Taita. Kufuatia uhuru wa Kenya mwaka wa 1963, uwindaji ulipigwa marufuku katika mbuga hii na usimamizi wa Tsavo ulisalimishwa kwa mamlaka ambayo hatimaye ikawa Kenya Wildlife Service. Tsavo sasa huvutia watalii wanaopiga picha kutoka kote duniani wenye riba ya kushauku upana wa jangwani na Mandhari ya ajabu.

Upandaji Mlima[hariri | hariri chanzo]

Cliffs Tembo chini Kitchwa saa alfajiri.

Mwaka wa 1978 Bill Woodley ambaye wakati huo alikuwa Mwangalizi wa Tsavo ya Magharibi, aliwaalika klabu ya Mountain Club of Kenya (MCK) ili kuchunguza maporomoko katika mbuga. Wapandaji poromoko hufurahia sana kuwaona tembo wakizurura nyanda chini ya maporomoko pamoja na kuwaona ndege aina ya mwewe, tai na kozi wakipepea huku mlima Kilimanjaro ikionekana vema. Upandaji mwamba ni baadhi ya utenzi bora nchini Kenya, ukuta mgumu wa gneiss mara nyingi hufunikwa na haina mimea. Nyufa na pembe kadhaa ziko, lakini huwa zinamimea nyingi. Kipande cha mwamba kinachovutia ziadi, cha urefu wa mita 300 high upande wa mashariki wa Kichwa Tembo, uliwavutia wapelelezi wa kwanza na kupelekea kuinuka kwa chemni ya Tsavo Kuu. Mastadon ilichukua ziara 3 kabla ya kukamilishwa. Njia ya hivi majuzi, Ivory Tower katika Miamba ya Ndovu (Elephant Rocks), ni kati ya upandaji mgumu na bora nchini Kenya. Kwa ujumla vigingi havifai kubebwa. Isipokuwa kupanda mwamba katika kivuli, watu hushauriwa kuanza kupanda mapema kwani joto jingi huwa wakati wa siku wazi.

Kibali walichopewa MCK kupanda mwamba, na kuweka kambi kando ya mto Tsavo, ni upendeleo maalum na kila juhudi lazima ifanyike ndiposa kusiwe na hali ya hatari kwa vitendo vya kutojali. Wapandaji wengine wanapaswa kuwasiliana na MCK ikiwa wanataka kupanda mlima huu.

Maelezo ya upandaji na taratibu yake: Rock Climbing Guide to Kichwa Tembo Archived 9 Mei 2008 at the Wayback Machine.

Tazama Pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]