Goregore
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
| Goregore | ||||||||||||||||
|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
| Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||
|
Goregore, gegemela au vinuka ni ndege wa jenasi Phoeniculus katika familia Phoeniculidae. Hawa ni ndege weusi wenye mkia mrefu na domo refu jekundu au jeusi lililopindika. Mwangani kwa jua manyoya yao yana mng'ao kijani au zambarau wa metali. Kuna mabaka meupe kwa mabawa na mkia. Hupenda kuwa kwa makundi na hupiga kelele pamoja mara kwa mara wakitetea. Inaelekea kama sauti yao ni asili ya jina “gegemela”. Hula wadudu ambao wanawatafuta katika nyufa za miti kama vigong'ota. Jike huyataga mayai 2-4 ndani ya tundu asilia ya mti au tundu ya zuwakulu au kigong'ota. Baina ya kundi la kama ndege kumi ipo jozi moja tu inayozaa. Ndege wengine wasaidia hawa wawili kutunza makinda.
[hariri] Spishi za Afrika
- Phoeniculus bollei, Goregore Kichwa-cheupe (White-headed Woodhoopoe)
- Phoeniculus castaneiceps, Goregore-misitu (Forest Woodhoopoe)
- Phoeniculus damarensis, Goregore Zambarau (Violet Woodhoopoe)
- Phoeniculus somaliensis, Goregore Domo-jeusi (Black-billed Woodhoopoe)
- Phoeniculus purpureus, Goregore Kijani (Green Woodhoopoe)